MKUU WA MKOA WA NJOMBE ATAKA TRA NA TFDA WASHIRIKIANE AKIWA KATIKA ZIARA YA KUTEMBELEA MABANDA YA NANE NANE MBEYA.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kepten Mstaafu Aseri Msangi akipata maelezo mbali mbali katika Banda la Tanseed.
Kaimu Meneja wa TFDA Kanda ya Nyanda za juu kusini Rodney Alananga akimuonesha Mkuu wa Mkoa baadhi ya bidhaa feki ambazo hazifai kwa matumizi ya binadamu.
Mkuu wa Mkoa akiangalia kiroba cha Konyagi kilichobandikwa nembo feki ya TRA.
Afisa
elimu kwa Mlipa kodi (TRA)wa Mkoa wa Iringa, Masunga Faustine
akikichunguza kwa makini kiroba cha Konyagi ili kuangalia namna
ilivyochakachuliwa.
Maafisa wa TRA wakifafanua jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
***************
MKUU
wa Mkoa wa Njombe, Kepteni Mstaafu Aseri Msangi, ameziagiza Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya udhibiti wa chakula na dawa(TFDA)
kuwa na mahusiano ya karibu.
Agizo
hilo alilitoa jana katika ziara ya kutembelea mabanda ya maonesho ya
wakulima nanenane yanayoendelea katika viwanja vya John Mwakangale
jijini Mbeya.
Msangi
alisema kukiwa na mahusiano mazuri baina ya mamlaka hizo mbili
kutachangia kudhibiti uingiaji na matumizi ya bidhaa feki hapa nchini.
Aidha
alilazimika kutoa agizo hilo baada ya Tfda kubaini matumizi ya nembo ya
TRA katika vinywaji vikali vinavyozalishwa na Konyagi kutumika katika
pombe feki.
Katika
ziara hiyo ambayo Mkuu wa Mkoa huyo alipitia mabanda ya Tra na Tfda
alibaini kutokuwa na mahusiano na ushirikiano kutokana na Afisa wa Tra
kushindwa kuigundua nembo yao kama ni Feki.
Akifafanua
mbele ya Mkuu wa Mkoa kuhusu pombe feki, Kaimu Meneja wa TFDA kanda ya
Nyanda za juu kusini, Rodney Alananga, alisema mbali na Serikali kupiga
marufuku uingizwaji na matumizi ya Pombe kali kutoka nje ya nchi lakini
pia imegundulika kuchakachuliwa kwa pombe za ndani.
Alananga
alitolea mfano ni pombe aina ya Konyagi inayozalishwa na kampuni ya
Tanzania Distillers Limited(TDL)kuwa wafanyabiashara wanafoji nembo ya
TRA inayopaswa kubandikwa kwenye chupa na karatasi la kinywaji hicho.
Alizitaja
baadhi ya sifa zilizokutwa katika pombe iliyochakachuliwa kuwa ni
pamoja na utoafuti wa ujazo ulioandikwa kwenye nembo ya TRA na Nembo ya
Kiwanda ambapo Kiwanda kimeandika ujazo wa ml 100 na kwenye nembo
ikisomeka Ml 10.
Tofauti
zingine ni pamoja na kutofautiana kwa jina la kiwanda, jina la bidhaa
na biashara kukosekana kwa tarehe ya kuanza kutumika na mwisho wake
pamoja na nembo hiyo feki kufutika kirahisi kuliko nembo halisi.
Kwa
upande wake Afisa Elimu kwa Mlipa Kodi Mkoa wa Iringa, Faustin Masunga,
alikiri kutojua tofauti hizo na kuahidi kuzidi kutoa elimu kwa wananchi
ili kuepuka kuhatarisha afya za watu.
Hata
hivyo Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Kapt Mstaafu Aseri Msangi aliiagiza
Mamlaka ya mapato (TRA) kujikita katika uoaji wa elimu kwa wanunuzi na
walaji ili kuongeza ukusanyaji wa mapato.
Alisema
endapo mnunuzi ataelimishwa juu ya sheria ya kodi(EFD Regulation ya
Mwaka 2010) ya kumtaka anaponunua kitu adai risiti itasaidia kuongeza
kwa ukusanyaji wa mapato nchini.
Alisema
katika utoaji wa elimu wanapaswa kufuata mfumo wa Serikali ambao hutaka
kumshirikisha kuanzia ngazi ya kijiji hadi ngazi za juu ambao ndiyo
wenye watu na wanaopaswa kukusanya watu endapo watataka kutoa elimu.
Katika
ziara hiyo Mkuu huyo wa Mkoa pia alitembelea mabanda ya kuzalisha mbegu
ya Tanseed, Bodi ya Pareto,Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe,
Mamlaka ya hali ya hewa na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.
Comments