MWANAMKE ALIYEPIGWA BOMU NA POLISI AKATWA KIGANJA CHA MKONO WA KULIA JIJINI DAR ES SALAAM.


Mkazi wa Mbagala Zakhiem, Dar es Salaam, Mwanaharusi Hamisi akionyesha mkono wake wa kulia uliokatika kiganja baada ya kulipukiwa na kitu kinachodaiwa kuwa bomu la machozi lililorushwa na Polisi waliokuwa wakiwatawanya wananchi waliokuwa wakifanya fujo eneo hilo. Habari zaidi Uk5. Picha na Venance Nestory.


Dar es Salaam. Mkazi wa Mbagala Zakhiem, Mwanaharusi Hamis amepoteza kiganja chake cha mkono wa kulia baada ya kulipuliwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu lililorushwa na polisi wakati wakitawanya wananchi.


Mwanaharusi alilipuliwa na bomu hilo Agosti Mosi 2014, saa 3:00 usiku alipokuwa anatoka ndani kwenda msalani.


Akizungumza na gazeti hili jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Wodi ya Mwaisela namba mbili alikolazwa, alisema tukio hilo limebadilisha kabisa mustakabali wa maisha yake.


Mwanaharusi, ambaye ni mama wa watoto wawili alisema alikumbwa na madhila hayo wakati polisi walipokwenda mtaani kwao kumkamata mtuhumiwa wa wizi wa pikipiki. Alisema walipofika, vijana waliokuwa maeneo hayo waliwarushia polisi mawe, ndipo polisi walipofyatua mabomu ya machozi na risasi kuwatanya wananchi hao.


“Ilikuwa saa 3:00 hivi mimi na watoto wangu tukiwa ndani hatujui nini kinachoendelea nje, ghafla tulianza kusikia milio ya risasi na mvumo wa kitu kuelekea upande wa ilipo nyumba yetu. Wakati huo nilikuwa natoka ndani kwenda msalani, nikaona kitu kimenipiga na kunichana sehemu za mkono na miguuni, baadaye nikagundua kilichonipiga kilikuwa bomu,” alisimulia Mwanaharusi.


Alisema baada ya tukio hilo polisi walimpelekea kituoni kwa ajili ya kupata fomu namba ya tatu ya matibabu (PF3) na baadaye Hospitali ya Temeke, alikopewa rufaa ya kwenda Muhimbili kwa kuwa alikuwa akitoka damu nyingi.


“Nimechanganyikiwa. Mimi ndio mtafutaji wa familia, mwanangu wa kwanza amemaliza kidato cha nne na wa pili ana miaka tisa,” alisema.


Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Temeke, Kienya Kienya alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema ufafanuzi utatolewa leo na kamanda wa Kanda ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova.MWANANCHI

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.