ANAYELITAKA JIMBO LA WILLIAM LUKUVI AWA MAKAMU MWENYEKITI WA BAVICHA

Patrick Ole Sosopi
YULE kijana anayetarajia kutoa upinzani mkali kwa William Lukuvi endapo chama chake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kitamsimamisha kuwania ubunge Jimbo la Isimani katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Patrick Ole Sosopi amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Bara wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema(BAVICHA). Mbali na kuwa mbunge wa Jimbo la Isimani kwa awamu ya tatu sasa, William Lukuvi ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (sera na uratibu wa bunge). Katika uchaguzi huo wa BAVICHA uliofanyika jana jijini Dar es Salaam, nafasi ya Mwenyekiti ilikwenda kwa Patrobasi Katambi na Zeudi Abdalla alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Zanzibar. 

Kuchaguliwa kwa Sosopi kushika nafasi hiyo nyeti ndani ya chama hicho kumeelezwa na baadhi ya wafuatiliaji wa siasa za mkoa wa Iringa kwamba kunamuongezea nguvu kisiasa. 
Patrick Ole Sosopi ambaye ni baba wa mke mmoja na mwenye mtoto mmoja, ni mmasai aliyezaliwa na kukulia mkoa Iringa, jimbo la Ismani. 
Ana umri wa miaka 28. Ni msomi wa shahada ya kwanza ya Biashara na Utawala (rasilimali watu) kutoka chuo kikuu cha Ruaha (RUCO). Kwa sasa kazi zake ni kufuga ng'ombe. 
Historia yake ya uongozi ilianzia akiwa shule ya msingi, sekondari hadi chuo kikuu cha RUCO ambapo alikuwa waziri wa Fedha kwenye serikali ya wanafunzi 2011/2012. 
Alijiunga rasmi na CHADEMA mwaka 2009 alipokuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza akiamini ni chama pekee ambacho kina tija ya kuboresha maisha ya jamii yake ya kimasai na changamoto mbalimbali ambazo zilikuwa zikiwakabili. 
Aliaminiwa na vijana wa Ismani na kupata kura zote bila kupingwa na kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA jimbo la Ismani. Baada ya kushauriwa na kushauriana na familia yake na vijana mbalimbali kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania, aligombea nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa BAVICHA Bara na ameshinda. 
Ingawa ni mojawapo wa wasomi wachache kwenye jamii yao ya kimasai, ni mtu ambaye usomi wake haujamfanya asahau mila na tamaduni za kimasai. Chakula chake, mavazi yake, desturi yake ya maisha ya kila siku ni desturi za kwao na zenye kuhuwisha Utanzania. BONGOLEAKS

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.