THE
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Fax: 255-22-2113425 |
|
PRESIDENT’S OFFICE,
STATE
HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,
Jumatano, Septemba 10, 2014, amefanya mazungumzo ya faragha na mgeni wake, Rais
Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Ikulu, Dar Es salaam.
Rais
museveni ambaye alikuwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika Tanzania,
aliwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kiasi cha saa 4
na dakika 10 asubuhi na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais Kikwete.
Mazungumzo
kati ya viongozi hao wawili, yalianza saa tano unusu asubuhi na kuchukua kiasi
cha saa moja na dakika 15.
Rais
Museveni aliondoka Ikulu baada ya chakula cha mchana na aliagana na mwenyeji
wake, Rais Kikwete kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar Es salaam, kabla
ya kupanda ndege yake kurejea nyumbani.
Imetolewa
na;
Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es
Salaam.
10
Septemba , 2014.
Comments