RAIS KIKWETE, MUSEVENI WALONGA FARAGHA KWA ZAIDI YA SAA MOJA IKULU



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425


Coat of Arms
PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatano, Septemba 10, 2014, amefanya mazungumzo ya faragha na mgeni wake, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda, Ikulu, Dar Es salaam.
Rais museveni ambaye alikuwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika Tanzania, aliwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kiasi cha saa 4 na dakika 10 asubuhi na kupokelewa na mwenyeji wake, Rais Kikwete.
Mazungumzo kati ya viongozi hao wawili, yalianza saa tano unusu asubuhi na kuchukua kiasi cha saa moja na dakika 15.
Rais Museveni aliondoka Ikulu baada ya chakula cha mchana na aliagana na mwenyeji wake, Rais Kikwete kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar Es salaam, kabla ya kupanda ndege yake kurejea nyumbani.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
10 Septemba , 2014.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI