NHC YAPANIA KUENDELEZA MKOA WA RUVUMA




 Uongozi wa Shirika la Nyumba la Taifa na wa wilaya ya Namtumbo ukitoka nje ya Ofisi ya Mkuu hiyo, baada ya kufanya mazungumzo ya kina ya mpango ya kujenga nyumba za gharama nafuu. PICHA ZOTE NA MUUNGANO SAGUYA WA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu na ujumbe wake wakiwa na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Bw. Abdulah Lutavi akiwatembeza kwenye eneo lililotengwa na Wilaya hiyo kwa ajili ya kujengewa nyumba na NHC. Shirika la Nyumba litajenga nyumba za gharama nafuu katika halmashauri hiyo hivi karibuni.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu, Mkuu wa Wilaya Natumbo, Bw. Abdulah Lutavi na ujumbe wao wakijadiliana kwenye eneo litakalojengwa nyumba za gharama nafuu na Shirika la Nyumba.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu na msafara wake wakikagua mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu wa Mkuzo, Songea. Mradi huo una jumla ya nyumba 18.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu akitembelea nyumba za Shirika za gharama nafuu zilizojengwa eneo la Mkuzo, Songea.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu akizugumza na Watendaji wa Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma kuhusu mpango wa NHC wa kuwekeza ujenzi wa nyumba katika halmashauri hizo.

 Sehemu ya Watendaji wa Halmashauri za mkoa wa Ruvuma wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu (hayuko pichani) alipozungumza na mkoa huo kuonyesha jia ya kujenga nyumba katika mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu akiongea na Watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma na Shirika la Nyumba la Taifa na kulihakikishia Shirika kupewa viwanja vya kujenga nyumba katika halmashauri zote za mkoa huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu akiangalia ufyatuaji wa matofali wa vikundi vya vijana Peramiho vilivyosaidiwa mashine hizo na NHC.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu akisikiliza maelezo ya kiongozi wa kikundi cha vijana Peramiho.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu akishiriki katika ufyatuaji wa matofali na vikundi vya vijana wilayani Peramiho mwishoni mwa wiki.
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu ukitembezwa katika maeneo yenye viwanja katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mwishoni mwa wiki.

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu akionyeshwa ramani ya eneo walilokabidhiwa na halmashauri ya Mbinga
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu na ujumbe wake wakionyeshwa viwanja na Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, Bw. Julius Mwakafwila vitakavyotumika kujenga nyumba za gharama nafuu.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Bw.  Nehemia Mchechu katika picha ya pamoja na Watendaji wa wilaya ya Mbinga na NHC wakati akiagana na ujumbe wa Halmashauri ya Mbinga mwishoni mwa wiki

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU