VETA NYANDA ZA JUU KUSINI YATANGAZA VYUO VILIVYOSAJILIWA NA VETA MKOA WA IRINGA



Kaimu  mkurugenzi wa VETA nyanda za juu kusini Bi Suazana Magani  akizungumza na  wamiliki wa vyuo 30 mkoa wa Iringa vilivyopatiwa usajili wake leo 
Mratibu wa VETA kanda ya nyanda za juu  kusini Bw Jonh Mwanja akionya vyuo  bubu mkoani Iringa 
Baadhi ya  wakuu wa vyuo vilivyosajiliwa mkoa wa Iringa 
Wakuu wa vyuo  Iringa  wakifuatilia maelekezo ya viongozi wa VETA kanda ya nyanda za juu kusini 
Mkuu wa chuo  cha Mufindi VTC Bw Fredy Kigola kulia akiwa na  wakuu  wenzake wa vyuo mbali mbali Iringa 
Mkuu wa  chuo  cha Mufindi VTC Bw Fredy Kigola akikabidhiwa  cheti na kaimu mkurugenzi wa Veta nyanda za juu kusini Bi Suzana Mgani leo baada ya  chuo  chake  kuwa kimoja wapo kati ya  vyuo 30 vilivyosajiliwa na VETA mkoa wa Iringa 
Mkuu  wa chuo  cha cha   Utalii Ruaha Bw Yohanes Sanga akikabidhiwa  cheti chake na kaimu mkurugenzi wa Veta nyanda za juu kusini Bi Suzana Mgani kulia ni mratibu wa Veta nyanda za juu kusini Bw John Mwanja 
Mkuu wa  chuo  cha Don Bosco Iringa akikabidhiwa  cheti 
Kaimu mkurugenzi  wa VETA nyanda za juu kusini Bi Suzana Mgani (mwenye gauni jekundu ) akiwa na mratibu wa VETA kanda ya nyanda za juu kusini Bw John Mwanji wa tano  kutoka kushoto mbele ,wengine ni  wakuu wa  vyuo 30 mkoa wa Iringa waliopewa vyeti vya usajili wa  vyuo  vyao 
Na  Francis Godwin Blog
CHUO  cha ufundi  stadi (VETA ) nyanda  za  juu kusini imetangaza vyuo  30  vilivyosajiliwa na  vyenye sifa ya  kutoa elimu ya mafunzo mbali mbali  yakiwemo  ya Hoteli na utalii mkoa  wa Iringa na  kuwataka wazazi  kutopeleka watoto  wao katika  vyuo visivyosajiliwa na VETA.

Akitangaza  vyuo  hivyo vyenye  sifa ya  kuendelea  kutoa   mafunzo mbali mbali  leo  mbele ya wanahabari na  wamiliki wa  vyuo  hivyo  vilivyosajiliwa  mkoani hapa jana  kaimu mkurugenzi wa VETA nyanda za juu kusini Bi Suzana Magani  alisema kuwa  lengo la  kuvitangaza  vyuo  hivyo ni kutaka kuepusha utapeli ambao   wazazi  na  wanafunzi  wamekuwa  wakikutana  nao kutoka katika  baadhi ya  vyuo ambavyo havitambuliwi na VETA.

Hivyo  alisema  kuwa kuanzia  sasa ni vema  wazazi  kuepuka  kupeleka  watoto  wao  katika  vyuo ambavyo havitambuliki na VETA  kwani  kufanya  hivyo ni sawa na kupoteza fedha na muda wa  mtoto  kuwepo katika chuo kisichotambulika.

" VETA ilifuta  usajili wa usajili wa  vyuo  vyote  mwaka 2009  na mwaka 2010 ilifanya  ukaguzi kwa  vyuo  vyote na mwaka huu 2014 imeanza  kutoa vyeti  vya usajili kwa  vyuo  ambavyo  vinasifa  ya  kuitwa  vyuo  vya ufundi na vyuo vya kutoa mafunzo ya hoteli na utalii katika mikoa yote nchini na katika mkoa  wa Iringa hadi  leo Septemba 12  ni  vyuo 30  pekee  ndivyo  vyenye sifa ya  kuitwa  vyuo" alisema mkurugenzi huyo

Kuwa kwa muda  wote  huo  baada ya  vyuo hivyo kufutiwa  usajili VETA   kilikuwa na jukumu la kutoa mafunzo mbali mbali  ya uboreshaji wa  vyuo kwa  wamiliki wa  vyuo  hivyo na   hadi sasa wamiliki wa vyuo 30  pekee  ndio  wamefanikiwa kuviwezesha  vyuo  vyao kuwa na sifa ya kuitwa  chuo .

" Hivyo wito  wangu kwa  wamiliki  wote wa vyuo ambavyo  leo  mmepata  usajili  wa kudumu na VETA jambo ambalo mnapaswa  kufanya kuanza  kuvitangaza  vyuo vyenu  katika   vyombo mbali mbali  vya habari ili kuwanusuru  wazazi na  wanafunzi  wanaoendelea  kurubuniwa na vyuo visivyo na  sifa na havitambuliwi na VETA"

 Alisema kuwa  kuvitangaza  vyuo  hivyo na fani  zinazotolewa kutasaidia wazazi  kuchagua  chuo  cha  kumpeleka mtoto  kupata  elimu   na kuwa  usajili  huo kwa chuo unapaswa  kuwa ni usajili endelevu na sio  chuo toka kimesajiliwa  hakina kozi mpya  zaidi ya kuendelea na kozi za  zamani na madaraja  yale yale "

Hivyo  alisema usajili  huo unapaswa kuwa endelevu kwa  kubuni kozi mpya  kulingana na miaka  inavyosonga  mbele .

Bi Mgani  aliwataka  wamiliki wa  vyuo  ambavyo havijasajiliwa  kufika  kusajili  vyuo  vyao kabla ya  ofisi yake  kuanza msako  wa  kuvifungia vyuo  hivyo kama  ilivyofanyika katika mkoa wa Ruvuma na Njombe .

Alivitaja   vyuo bora 30 ambavyo  vimesajiliwa katika mkoa wa Iringa  na  kuwataka wazazi kuepuka na  vyuo bubu ambavyo havitambuliki na  VETA  kuwa ni pamoja na  Mufindi VTC, Ifunda Technical Secondary School , Mgongo Catholic VTC, Amani VTC, Mafinga Secretarial College, Nyabula VTC, KIlolo VTC, Isimani VTC, Sanaa House VTC, Matumaini Centre  VTC, Incoment VTC, Mafinga Lutherani VTC, Kibidula Agriculture VTC,  na Ifunda Mission VTC

Vingine ni   Cory Training College, Ilula Institute of  Technology and Business Studies , Starcom Hotel Academy ,Ruaha Tourism College , Southern College of Tanzania , Tabez VTC, Ng'ingula VTC, ST. Jerome VTC, Ulete VTC, Upendo VTC, ST. Therese VTC,ST Maria Goreett VTC, SCim Brothers VTC, Nyota ya asubuhi VTC na Don Bosco Youth Trainging Centre 

Kwa  upande  wake mratibu  VETA nyanda  za  juu kusini Bw  John Mwanja  alisema kuwa  wazazi  wasidanganyike na utapeli  unaofanywa na  baadhi ya wamiliki wa  vyuo  kwa kutangaza  kuwa  wanatoa Dimploma na  kuwa  katika mkoa wa Iringa zaidi ya  vyuo  vikuu kama cha Iringa  na Ruaha na kile  cha Iringa  RETCO Bussiness hakuna  chuo  chenye sifa ya  kutoa Diploma ndani ya  mkoa wa Iringa .

Hata  hivyo  alisema kuwa hakuna  chuo  kinachosajiliwa NECTA bila ya  VETA kujua  na kuwa  vyuo  vinavyodai  vimesajiliwa na NECTA ni utapeli  wa hali ya  juu kwani  hadi  sasa VETA imewasiliana na NECTA makao makuu   hawavitambui vyuo  hivyo na  kuwa  kuendeelea kutoa  elimu bila kusajiliwa ni  wizi na mmiliki anapaswa  kuwajibishwa  kisheria na  wao kama VETA baada ya kuhitimisha  zoezi hilo  watatoa ripoti katika  vyombo  husika vya kisheria  ili  kuchukua hatua  juu ya vyuo  hivyo.

Alisema baadhi ya  vyuo hivyo  feki vimekuwa  vikitoa  elimu  ya chuo  bila ya kuwa na mtaala wa VETA na  wengi  wanatumia uzoefu  wao walioupata na  sio sifa za zinazotambuliwa na VETA.


Mkuu  wa  chuo  cha Mufindi VTC Bw Fredy Kigola  mbali ya kuipongeza VETA kwa  mafunzo mbali mbali  wanayoyatoa  bado  alisema kuwa ubora wa  elimu hauwezi kufanikiwa iwapo watoto  watafundishwa katika vyuo feki na   kudai kuwa chuo chake  kimeendelea  kupata umaarufu  mkubwa kwa  wazazi kutoka nje na ndani ya Mufindi kupeleka watoto katika  chuo  hicho kutoka na ubora wa mafunzo yanayotolewa  baada ya VETA kuwapa  elimu ya ziada.

Kigola  alisema kuwa  uamuzi wa VETA wa kuvifunga  vyuo bubu utasaidia kuboresha mafunzo kwa  wanafunzi  wanaosoma katika  vyuo  hivyo .

Wakati mkuu wa chuo cha  cha Utalii Ruaha Bw Yohanes Sanga akitaka wakuu wa  vyuo  vilivyosajiliwa mkoani Iringa kuungana kwa kuanzisha chama  chao  ili  kinapoibuka chuo kisichosajiliwa  kuweza kupaza sauti ya pamoja.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI