BENKI YA CRDB YAZINDUA WIKI YA HUDUMA KWA MTEJA


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), akiwa na  Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay wakati wakiingia katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya serena jijini Dar es Salaam kuzungumzia Wiki ya Wateja wa Benki hiyo itakayoanza Oktoba 6-11. 
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (kulia), akiingia katika mkutano huo akiongozana na maofisa wa Benki hiyo.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (katikati) wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei muda mfupi kabla ya kuanza mkutano na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika picha ya pamoja.
 Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa jkatika mkutano huo.
 Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo.
Baadhi ya Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika mkutano huo.


Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, anayeshughulika na Uendeshaji na Huduma kwa Wateja, Saugata Bandyadhiyay (kushoto) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu (kulia) akiwa na maofisa wa Benki hiyo kabla ya kuanza kwa mkutano.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei kuzungumza na waandishi wa habari kjuhusu Wiki ya Wateja wa Benki ya CRDB.



Mkurugenzi wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu maadhimisho ya wiki ya Wateja wa Benki ya CRDB itakayoanza Oktoba 6-11.
 
Na Mwandishi Wetu


WATANZANIA wametakiwa kutumia huduma za kibenki katika kukuza na kujiongezea uchumi wa maisha yao.



Rai hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei katika mkutano wake na waandishi wa habari kuhusu wiki ya wateja wa benki hiyo itakayoanza Oktob 6,hadi 11,mwaka huu.


Alisema wiki hiyo ni maalum kwa ajili ya kusikiliza kero mbalimbali za wateja ikiwemo kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa.

"Azma kubwa ya maazimisho hayo ni kuwasikiliza wateja na kutimiza mahitaji yao kwa wakati ...lengo la CRDB ni kuboresha na kuinua uchumi wa kila mtanzania kupitia mikopo, kutunza na kukuza amana pamoja na kutoa ajira kwa vijana na misaada kwa jamii"alisema Dk. Kimei.

Akifafanua zaidi alisema kwa kutambua umuhimu na mchango mkubwa wa watanzania kwa CRDB, wanatumia wiki hiyo kutoa huduma bora na kusikiliza kero zao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*