Benki ya Exim katika Maonyesho ya Wiki ya Viwango yaliyoandaliwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS)
Afisa
Mauzo wa Benki ya Exim Tanzania, William Kikoti (wa pili kushoto),
akimkaribisha Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw.
Odilo Majengo (kulia), katika banda la benki hiyo wakati wa Maonyesho ya
Wiki ya Viwango yaliyoandaliwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS)
katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam Jumatano. Waliopo
katika banda hilo ni Mkuu wa Matawi wa Benki ya Exim, Bi. Elizabeth
Majengoh (kushoto) na wafanyakazi wengine wa benki hiyo. Picha na mpiga
picha wetu. Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Bw. Joseph
Masikitiko (kushoto), akifurahia jambo wakati akipata maelezo kutoka kwa
Mkuu wa Matawi wa benki ya Exim, Bi. Elizabeth Majengoh (wa pili
kulia), juu ya huduma na bidhaa zitolewazo na benki hiyo, alipotembelea
banda la benki hiyo katika Maonyesho ya wiki ya viwango yaliyoandaliwa
na TBS na kufanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam
Jumatano. Pamoja nao ni Mkuu wa Matawi wa benki hiyo Agnes Kaganda
(wakwanza kushoto) na wafanyakazi wengine wa benki hiyo. Picha na mpiga
picha wetu. Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Bw. Joseph
Masikitiko (kulia), akiwasalimia wafanyakazi wa Benki ya Exim
alipotembelea banda la benki hiyo katika Maonyesho ya Wiki ya Viwango
yaliyoandaliwa na TBS na kufanyika katika viwanja vya Karemjee jijini
Dar es Salaam Jumatano. Picha na mpiga picha wetu. Afisa
Mauzo wa Benki ya Exim, Bw. William Kikoti, akifafanua juu ya bidhaa na
huduma mbalimbali zitolewazo na benki hiyo kwa baadhi ya washiriki
waliohudhuria maonyesho ya wiki ya viwango yaliyoandaliwa na Shirika la
Viwango Tanzania (TBS) katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam
Jumatano. Wengine ni wakuu wa watawi wa benki hiyo Bi. Elizabeth
Majengoh (wapili kushoto) na Bi. Agnes Kaganda (aliyekaa wakwanza
kulia). Picha na mpiga picha wetu.
Comments