Baada ya
Ushindi wa Redds Miss Tanzania 2014 kuangukia kwa mwanadada Sitti Abbas
Mtemvu, maneno yalizagaa sana kuwa mrembo ana miaka 18 na ana Shahada ya
Uzamili (Masters).
Katika
kuondoa utata, Katibu wa kamati ya Miss Tanzania Bosco Majaliwa amesema
kuwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu amezaliwa Mei 31 mwaka
1991 na umri wake sahihi ni miaka 23 na sio miaka 18 kama ilivyozagaa
sehemu mbalimbali.
Katibu
huyo aliongeza kuwa Sitti ana Shahada ya ya Uhusiano wa Kimataifa na
alimaliza masomo yake Desemba mwaka jana katika Chuo Kikuu cha North
Texas kilichoko kwenye jiji la Dallas nchini Marekani.
Sitti
Mtemvu bado hajasoma ngazi ya Shahada ya Uzamili (Masters) kwa sasa ila
anatarajiwa kwenda kusoma ngazi hiyo huko nchini Marekani.
Comments