Mmoja wa washiriki wa Semina ya Fursa akiuliza swali kwa Meza kuu ya watoa mada kuhusiana na mradi wa ufugaji wa kuku.
Mwakilishi
kutoka Shirika la Taifa la hifadhi ya Jamii (NSSF),Bwa.Ally Mkulemba
akizungumza faida mbalimbali za kujiunga na shirika hilo la NSSF,alisema
kuwa vijana wanapaswa kuamka kwa sasa na kuanza kuzichangamkia fursa
zitokanazo na shirika hilo,ikiwemo mikopo,bima ya Aya na mengine kwa
maendeleo na ujenzi wa maisha bora
Msanii
wa Bongofleva Baba Levo,ambaye pia ni mmoja wa mabalozi wa shirika hilo
la NSSF,akielezea yeye na wasanii wenzake wanavyonufaika na fursa
mbalimbali zipatikanazo na shirika,Baba Levo amewataka wasanii
mbalimbali ambao bado hawajajiunga na shirika hilo wakiwemo na vijana
mbalimbali wafanye hivyo sasa,kwani shiriki hilo linatoa fursa nyingi za
kuwawezesha vijana kuwapa wigo mkubwa wa kutimiza ndoto za maisha yao
Baadhi ya Washiriki wa Semina ya Kamata
Fursa,Jitathimini,Jiamini,Jiongeze wakimsikiliza Msanii mahiri wa Mashairi pichani,Mrisho Mpoto,alipokuwa akizungumza
ndani ya moja ya ukumbi wa hoteli ya KBH,ilioko nje kidogo ya mji wa
Singida.Semina ya Fursa 2014 inaandaliwa na Waandaaji wa Tamasha la
Fiesta 2014 linalotarajiwa kufanyika leo usiku ndani ya uwanja wa Namfua
mjini Singida.
Comments