Pichani juu na chini ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akikata utepe kuzindua rasmi mradi mkubwa wa maji wa kwa vijiji vya Noondoto na Elang’atadapash uliosaidiwa na UNDP. Kushoto ni Mratibu Kitaifa kutoka UNDP, Bw. Nehemia Mususuri akishuhudia tukio hilo.
Jiwe la msingi kama linavyosemeka pichani.
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na wakazi wa vijiji vya Noondoto na Elang’atadapash mara baada ya kuzindua mradi huo wa maji.
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez, akinawa mikono na maji hayo mara baada ya kuzindua rasmi tangi kubwa la maji kijijini hapo.
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez, akimtwisha ndoo ya maji mkazi wa jiji cha Elang’atadapash, Bi. Nabulu Kumokndare kama ishara ya kuzindua rasmi mradi huo.
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez, akikagua kisima cha maji cha kijiji hicho.
Wanyama wakinywa maji safi na salama wakati wa sherehe za kuzinduliwa rasmi kwa mradi mkubwa wa maji utakaohudumia wakazi 9,700 na mifugo 47,700.
Comments