HITILAFU YA UMEME KWENYE LIFTI YASABABISHA TAFRANI BENKI YA NBC DAR

 Baadhi ya wafanyakazi wa  Benki ya NBC, wakivuka barabara kurejea tena ofisini baada ya kuzikimbia kutokana na hitilafu ya umeme iliyotokea kwenye lifti ya dharula katika Makao Makuu ya benki hiyo, makutano ya mitaa ya Sokoine Drive na Azikiwe, Dar es Salaam leo. Hitilafu hiyo iliyotokea majira ya saa 3:30, ilisababisha tafrani kiasi cha wafanyakazi kuzikimbia ofisi kwenda Bustani ya Posta ya Zamani (picha ndogo).Wateja waliopatwa na zahama hiyo walielekezwa na uongozi kwenda kupata huduma kwenye matawi mengine ya benki hiyo. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Wafanyakazi wakiwa kwenye bustani ya Posta ya Zamani iliyopo mbele ya jengo lao, baada ya kumbia tafrani hiyo

 Wafanyakazi wa Benki hiyo wakirejea ofisini baada ya kuhakikishiwa usalama majira ya saa 4;35 asubuhi
 Wafanyakazi wa huduma ya kwanza wakiwa na vifaa vyao tayari kutoa huduma hiyo. Hata hivyo kwa mujibu wa Rukia Mtingwa alisema hakuna mfanyakazi wala mteja aliyeumia wakati wa tafrani hiyo.
 Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Rukia Mtingwa (katikati) akiwasilinana  na watu mbalimbali baada ya hali ya usalama kurejea
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC, Rukia Mtingwa (wa pili kulia) akizungmza na waandishi wa habari juu ya tafrani hiyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.