IDARA YA UHAMIAJI MKOA WA NJOMBE YATOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA WILAYANI MAKETE

Watoto yatima wakipewa zawadi na Idara ya uhamiaji mkoa wa Njombe
Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akiwa amembeba mtoto yatima anayelelewa kituo cha Nyumba ya yatima Bulongwa
Baadhi ya msaada uliotolewa
Mkuu wa wilaya akikabidhiwa msaada huo na afisa uhamiaji mkoa wa Njombe.

Hivi karibuni Idara ya uhamiaji mkoa wa Njombe iliunga mkono jitihada za mkuu wa wilaya ya makete Josephine Matiro kusaidia vituo vya watoto yatima wilayani humo kwa kutoa msaada wa zaidi ya shilingi milioni 1

Akizungumza wakati akikabidhi msaada wao afisa uhamiaji mkoa wa Njombe Rose Mhagama alisema wameguswa na suala hilo na kuamua kuvisaidia vituo vya watoto yatima Makete vitu mbalimbali, na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kuwasaidia watoto hao

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya Hiyo Bi Josephine matiro amewataka wanamakete kubadilika na kuacha dhana kuwa watoto hao watasaidiwa na wafadhili kutoka nje na badala yake nao wawasaidie watoto hao kwa kitu chochote walichojaliwa na Mungu

Vituo vilivyonufaika ni Nyumba ya yatima Bulongwa, Fema Matamba na Kituo kipya cha Kisinga

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI