Waziri
Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu
kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli
maalumu.
Waziri
Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu,
ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji,
amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete
akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri
na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.Katika barua yake
ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu
Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.
Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo
Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya
B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na
badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.Baadaye leo Pinda
alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.-BBC
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya
Utalii nchini, Devota Mdachi (kushoto) na Mwenyekiti wa Kampuni ya
Nakheel PSSC ya Dubai, Bw, Ali Lootan wakizungumza katika Mkutano wa
Kuitangaza Tanzania na kuvutia wawekezaji wa Dubai uliofunguliwa na
Waziri Mkuu mjini Dubai Desemba 17, 2014.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akiongozwa na Meneja Mkuu wa Shamba la kufuga
ng'ombe wa maziwa la Al Rawabi Dairy la Dubai, Dr. Ahmed Al Mansour
(kulia kwake) kukagua shamba hilo akiwa katika ziara ya kikazi nhini
humo Desemba 17, 2014
Waziri
Mkuuu, Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka kwa Meneja mkuu wa shamba la
kufuga ng'ombe wa maziwa la Al Rawabi Dairy la Dubai, Dr. Ahmed Al
Mansour (kulia) wakati alipotembelea shmaba hilo akiwa katika ziara ya
kikazi nchini humo Desemba 17, 2014.
Comments