Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Iringa HASSANI MTENGA akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Kihesa Mgagao.
Baadhi ya wananchi waliohudhulia mkutano huo.
NA FREDY MGUNDA,KILOLO
Katibu wa Chama cha Mapinduzi
CCM mkoani Iringaha HASSANI MTENGA, amefungua rasmi kampeni za uchaguzi
wa Serikali za mitaa katika kijiji cha kihesa mgagao na kulakiwa na
mamia ya wananchi katika kijiji chicho kilichpo wilayani kilolo.
Akizungumza wakati wa ufunguzi
wa kampeni hizo Katika Kijiji hicho HASSANI MTENGA alisema kuwa kampeni
hizo zinazotaraji kufikia kikomo Disemba 13 Mwaka huu, zilipaswa
kufanyika muda mrefu hivyo kilichochelewesha uchaguzi huo ni mchakato wa
upatikanaji wa katiba mpya.
MTENGA ametumia nafasi hiyo pia
kuwanadi mgombea nafasi ya uenyeviti wa kijij hicho ambapo amewaomba
wananchi wa kijiji hiocho kumchagua PHILIPO KAGINE awe mwenyekiti wao.
Akizungumzia sakata la vyama vya
upinzani kutaka kugomea uchaguzi amesema kuwa wasimamizi wa uchaguzi
nchini wanaangalia vigezo vya wagombea hivyo kama hawakuwa na vigezo
kusingekuwa na usamaria mwema kwenye kwenye jambo.
nao wananchi wa kijiji hicho
walimwambia katibu huyu kuwa mgombea wao kupitia chama cha mapinnduzi
atashinda kwa kishindo kwa kuwa kijiji hicho ni ngome ya CCM.
Comments