POLISI WAWILI WAUWAWA NEW YORK


Gari la polisi waliokuwemo polisi wawili waliouwawa mapema leo Brooklyn New York.
Polisi wa New York wakiwa eneo la tukio.
Na Mwandishi wa Vijimambo, New York
Polisi wawili wameuwawa mjini Brooklyn New Yrk na mtu ambaye inasemekana amesafiri toka Baltimore Maryland kwa kukusudia kufanya mauaji hayo na baadae kujipiga risasi baada ya kuzingirwa na polisi ndani ya kituo cha treni.

Polisi wawili waliouwawa Wenjan Liu na Rafael Ramos waliuwawa siku ya jumamosi mchana Desemba 20, 2014 wakiwa ndani ya gari lao wakiwa wameegesha mjini Brooklyn, New York wakiwa katika zamu yao ya kula lindo kwenye kazi yao ua upolisi.

Muuwaji huyo Ismaaiyl Brinsley miaka 28 aliwauwa polisi hao kwa kuwafyatulia risasi vichwani na sehemu ya mwili juu kifuani kupitia dirisha la abiria ya gari hiyo ya polisi iliyokua imeegeshwa kati ya mtaa wa Martle na Tompkins na polisi hao kufa papo hapo kwenye eneo la tukio huku muuaji akijipiga risasi na kufa baada ya kuzingirwa na polisi na baada ya kuona hakuwa na pakutokea.

Bwn. Brinsley inasemekana kusafiri kwake kuja kufanya mauaji hayo ya polisi ni kutokana na kutopatikana na kosa kwa polisi waliosababisha kifo na mmarekani mweusi  Eric Garner aliyekabwa koo na polisi waliokwenda kumkamata na baadae kupoteza maisha kwenye eneo la tukio japo mtuhumiwa huyo alikuwa akiwaambia polisi hao hawezi kupumua na polisi waliendelea kumkaba koo mpaka akapoteza maisha jambo lililowaudhi wamarekani weusi wengi akiwemo muuwaji wa polisi hao alifanya mauaji hayo kwa kukusudia kulipiza kisasi kwani alinukuliwa na vyombo vya habari akisema atakwenda Brooklyn New York kwa adhma ya kutekeleza nia yake hiyo

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA