FAMILIA YA MSWEMWA YATUMIA MILIONI 100 KUSAIDIA JAMII YA WANANJOMBE

Mkurugenzi  wa Hotel ya  Miriam Njombe  Bw Ditram Msemwa wa sita  kushoto akimpongeza  Bw Ngamanga  kwa  uzinduzi wa  kitabu  chake
Mkurugenzi  wa  Hotel ya  Miriam Njombe Bw Ditram Msemwa akizungumza katika hafla ya  kufunga mwaka
Baadhi ya  vijana  wanaonufaika na fursa   hiyo
Baadhi ya  wanafamilia na  wadau mbali  mbali
washiriki  wakifuatilia hafla  hiyo
Mkurugenzi wa taasisi ya  Mafanikio  foundation for  personal development na  mratibu  wa raslimali watu Bw Michael uhahula akitoa  maelezo  mafupi kabla ya  mgeni rasmi
Mgeni  rasmi  katika  hafla  hiyo  Adam Ngamanga  kutoka Afrika ya  kusini akifungua hafla hiyo
Mkurugenzi  wa  Hotel ya  Miriam akifuatilia hotuba  ya  ufunguzi
Baadhi ya  washiriki  wakiwa  katika  hafla    hiyo
baadhi ya  washiriki wa hafla hiyo  wakiungana na Mkurugenzi  wa Hotel ya  Miriam Njombe  Bw Ditram Msemwa wa sita  kushoto  akiungana na mgeni rasmi  Bw Ngamanga  kuzindua  kitabu  cha  Jitambue kilichoandikwa na Ngamanga wa katikati ,

Hiki ndicho  kitambu   cha  jitambue
Mwigizaji maarufu nchini Bw ras   katikati akiwa na  kitabu  hicho
Na Matukiodaimablog

KIASI  cha  Tsh  milioni 100  zimetumika   kusaidia   kusomesha  familia zenye  shida na  kutoa  mitaji ya  Tsh milioni 20  kwa  kila  kijana mwenye  ndoto ya  kujiendeleza  katika familia ya Msemwa na nje ya wanafamilia  hao wilayani Njombe mkoani Njombe.

 Akizungumza  katika hafla  fupi iliyofanyika  jana  katika  ukumbi wa  Hotel ya  Miriam Njombe mkurugenzi  wa Hotel ya  Miriam   Bw Ditram Msemwa alisema  kuwa  wameanzisha utaratibu   huo ambao  uliamnza  ndani ya  familia  kwa  dhana ya  kusaidiana  kimaisha  ila  kwa sasa  wameendelea  kupanua  wigo zaidi kwa  kusaidia jamii nyingine ya  wana Njombe.

"Tilianza kusaiodiana kama  familia kwa  kupeana  mitaji na  pesa za  kusomesha  watoto  ila  sasa  tumepanua  wigo kwa  kusaidia  wengine wa nje ya  familia na lengo letu kuona  Njombe inakuwa na  vijana  wasomi  wengi  zaidi"

Hata  hivyo wanamapango  wa kuanzisha  taasisi  kamili  ambayo  itafanya kazi  ya  kuisaidia jamii ya  wana Njombe  ili kuondokana na  dhana  iliyojengeka toka kwa  baadhi ya  viongozi ambao  wamekuwa  hawapendi  kurudi  kusaidia kwao  baada  ya kupata nafasi ya  uongozi.


Pia  mkurugenzi huyo alimpongeza  mkazi wa Njombe Bw Ngamanga  ambae  kwa  sasa anaishi  nchini Afrika ya  kusini kwa  kuendelea  kuwakilisha  vema  mkoa wa Njombe kwa  kutoa elimu kupitia  kitabu chake  cha  jitambue  ambacho  kimezinduliwa Njombe  na kutaka  vijana   wengine  kuiga mfano  huo .

Kuhusu  mitaji inayotolewa  alisema  kuwa  kila mwaka  wameweka  utaratibu wa  kutoa mtaji wa Tsh milioni 20 kwa  mtu mmoja  ili  kufanya  biashara  pamoja na  kusomesha   watoto  na  kuwa  toka  wameanza mpango huo  kiasi cha Tsh milioni 100  zimetolewa .






Click here to Reply, Reply to all, or Forward 16.62 GB (79%) of 21 GB used Manage ©2014 Google - Terms - Privacy Last account activity: 14 hours ago Details

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*