Madiwani wa Halmashauri ya Nsimbo washauriwa kupima afya zao

      

unnamed1
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mohamed Asenga Akifungua kikao cha baraza la madiwani mwishoni mwa wiki ,kulia kwake ni Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Diwani wa Kata ya Sitalike Slivester Nswima na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Said Juma Maraba.
unnamed2
Wataalam wakifuatilia kwa umakini mjadala wa  kikao cha madiwani Halmashauri ya Nsimbo
(Picha na Kibada Ernest-Katavi)
……………………………………………………………………………
Na Kibada Kibada –Katavi
Madiwani  wa  Halmashauri ya Nsimbo   Wilaya ya Mlele  Mkoa wa   Katavi   wameshauriwa kupima Afya zao na hasa  maambukizi ya VVU  kabla ya kuchukua fomu za kugombea Udiwani kwenye Kata zao  ili waweze  waweze kuwa mfano kwa watu wanaowaongoza na kutambua afya zao   kama kweli watakuwa na nguvu za kutosha kuwatumikia wananchi waliowachagua kwa kipindi cha kuwepo madarakani.
Diwani  wa Kata ya Kapalala  Reward Sichone alitowa ushauri huo   kwenye kikao cha Baraza la Madiwani   Halmashauri ya Nsimbo  baada ya kuwasilishwa kwa  taarifa ya kamati ya kuthibiti ukimwi iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa hiyo Diwani wa Kata ya Sitalike Silvester Nswima.
 Diwani Sichone alieleza kuwa ni  vizuri kwa madiwani  hasa wa Halmashauri  ya wilaya ya Nsimbo wanao tarajiwa kumaliza muda wao mwaka huu wakaandaliwa utaratibu na Halmashauri  wa kupimwa maambukizi ya VVU kabla ya kumaliza muda wao wa uongozi mwaka huu ili waweze kuwa mfano kwa watu wao wanao waongoza.
 Alilieleza Baraza hilo la  madiwani kuwa  endapo  watapimwa afya zao  mapema  itawafanya wajitathimini  kabla ya kuchukua fomu za kugombea  udiwani.
 Sichone alisema  endapo diwani atapimwa na kukutwa anamatatizo kwenye  afya yake  itamsadia  kuona kama kweli atakuwa na uwezo wa nguvu za kufanya kazi za wananchi  kwenye eneo lake.   
 Alifafanulia kuwa haitakuwa vizuri kwa diwani ambaye atapimwa na kukutwa  na maambukizi ya VVU  halafu  achukue fomu za kugombea tena wakati anajua kuwa hana nguvu za kufanya kazi za wananchi wake   hivyo swala la madiwani kupima  afya zao ni jambo la msingi sana
“Jamani mnacke lakini mambo haya ni muhimu sana katika jamii zetu hasa wananchi tunaowaongoza wakiona tunafanya namna hiyo wanakuwa na imani nasisi ingawa kupima siyo lazima ni hiari ya mtu “alisema Diwani Sichone.
 Kwa upande  wake Mwenyekiti  wa Kamati ya kudhibiti  Ukimwi  wa Baraza  la Madiwani  Sylvester Nswima  ambae ni Diwani wa Kata ya Sitalike alipinga  ushauri huo wa Diwani Sichone
Nswima alieleza kuwa  swala la Madiwani  kupimwa afya zao kwa pamoja  haiwezekani kwani kupima ni  hiyari ya kila mtu na sio lazima,hivyo kila mtu atapima kwa muda wake na kwa hiari yake.
Naye Mwenyekti wa  Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Assenga alisema   kitendo cha  madiwani kupima afya zao  kinaweza kuwa  ni mfano mzuri kwa watumishi  na wananchi wa Halmashauri ya Nsimbo kuona viongozi wao wakimwa afya   na kuwafanya nao wataiga mfano wa kupima mara kwa mara afya zao.
 Aliwatoa wasiwasi kwa kusema kuwa “Madiwani tusihofu kupimwa   bali tuangalie utaratibu wa  kuwaita wataalamu waje watupime afya  ili tuwe mfano kwa watu wengine  kwenye Halmashauri yetu  na Mkoa wa Katavi kwa ujumla wake”alisema Mwenyekiti Mohamed Assenga.
Katika taarifa ya utekelezaji wa shughuli za ushauri nasaha na upimaji wa VVU kwa hiariwalifanikiwa kupima watu 1221 kati ya wanaume 668 na  wanawake ni 551 ambapo kati ya watu hao waliopima waliokutwa na maambukizi walikuwa watu 36 kwa Halmashauri ya Nsimbo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI