Kada wa CCM mjini Iringa Bw Frederick Mwakalebela
katikati akiwa na Chritian Fwalo kulia (enzi za uhai wake )
walipokutana mjini Dodoma mwaka 2010 wakati mwakalebela alipokatwa
jina lake kugombea ubunge jimbo la Iringa mjini kushoto ni kada Ester Bulaya picha zote na maktaba ya matukiodaima Blog
ALIYEPITISHWA na vikao vya juu vya chama cha
mapinduzi (CCM) kugombea nafasi ya UNEC mkoa huo kuziba nafasi
iliyoachwa wazi na marehemu Lupyana Fute Bw Christian Fwalo ghafla .
Katibu wa itikadi na uenezi mkoa wa Njombe Nonaratus Mgaya aliueleza mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz kuwa Fwalo amefariki dunia juzi majira ya saa 12 jioni akiwa nyumbani kwake Njombe mjini. Mgaya alisema kuwa mwili wa Fwalo ameagwa jana mchana kabla ya kupelekwa kijijini kwao Uhalula mkoani humo kwa mazishi hapo yatakayofanyika leo (jumanne) Alisema kuwa kati ya wana CCM jaza fomu kuomba kuteuliwa kuwania nafasi ya UNEC mkoa wa njombe kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa MNEC wa mkoa huo aliyefariki dunia mwaka jana ,jina la Fwalo lilikuwa ni miongoni mwa majina matatu yaliyorudishwa .
Fwalo anzi za
uhai wake alikuwa ni mjumbe wa baraza kuu la UVCCMmkoa wa Iringa na
pia alikuwa na mpango wa kuja kugombea ubunge jimbo la Njombe
kusini katika uchaguzi mkuu mwaka huu kupitia CCM .
Mwenyekiti
wa UVCCM mkoa wa Iringa Tumain Msowoya akimzungumzia marehemu
Fwalo alisema kuwa kati ya vijana ambao walionyesha mchango mkubwa
katika jumuiya hiyo ni pamoja na marehemu huyo .
Kwani
alisema kuwa Fwalo kabla ya mkoa wa Iringa na Njombe kutengana
alikuwa ni kijana mwenye kujenga hoja na kuona jumuiya hiyo
inasonga mbele na siku zote alikuwa ni mshauri wa jumuiya hiyo.
|
Comments