Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova. ya
kuwakosesha amani wakazi wa Jiji la Dar es Salaam usiku wa Ijumaa
iliyopita, lile kundi la vijana wahalifu linalojulikana kwa jina la
Panya Road limefikia ukingoni baada ya kudhibitiwa kwa kasi kubwa na
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Amani linakupa ‘full
stori’.
TUJIUNGE NA KOVA
Akizungumza
na wanahabari wetu ofisini kwake jijini Dar juzi, Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema tangu siku ya tukio
hadi Jumatano (jana) ameendelea na msako maalum wa kuwadaka Panya Road
hao ambao ndiyo janga la mjini kwa sasa.
WANAE WAMMISI
“Nimeamua
haswa kuwafungia kazi, silali, wanangu wananimisi kwa muda, naingia
mzigoni usiku kucha kuhakikisha tunawakamata wahusika wote ambao
wanasadikika ni wafuasi wa Panya Road. Hata leo (Jumanne) na kesho
(Jumatano) msako upo palepale,” alisema Kova.
ALALA NJE SAA 120
Kutokana
na msisitizo huo wa Kova, hesabu za harakaharaka zinaonesha kuwa, tangu
Ijumaa iliyopita hadi Jumatano (jana), Kova atakuwa amelala nje kwa
siku 5 sawa na saa 120 ambapo muda wa asubuhi anakuwa ofisini kama
kawaida, jioni anaendelea na msako akisimamia vijana wake.
Kundi linalodaiwa ni Panya Road.
WALIOKAMATWA
Kwa
mujibu wa Kamanda Kova, hadi juzi Jumanne, idadi ya vijana 510
wanaotuhumiwa kuhusika na kundi hilo walikamatwa sanjari na viongozi wao
watatu.
“Ukiachilia
mbali wadogowadogo, vinara ambao tumewakamata ni Halfan Nurdini (24),
mkazi wa Tandale-Sokoni, Said Mohamed (22), mkazi wa Tandale-Sokoni na
Mohamed Ndangula mkazi wa Mburahati jijini Dar,” alisema Kova.
AMA ZAO AMA ZAKE
Akizidi
kutilia msisitizo kuhusu kundi hilo ambalo ni maarufu kwa kupora mali
za watu katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar, Kova alisema msako
unaendelea kwa wale wachache ambao bado hawajatiwa nguvuni basi ama zao
ama zake.
“Haiwezekani
vijana kama hawa watishie amani, niwaambie tu wale ambao bado
hatujawakamata, tutawafikia na wote tutawafikisha kwenye mikono ya
sheria,” alisema.
JK APELEKEWA TAARIFA
Imeelezwa
kuwa, kutokana na unyeti wa tukio hilo lililotikisa jiji kwa takriban
saa nne (Ijumaa), taarifa ya namna ambavyo linashughulikiwa zimepelekwa
Ikulu ya Magogoni kwa Rais Jakaya Kikwete ‘JK’ ambapo ametoa maagizo
mazito juu ya wahusika.
“JK
amepelekewa taarifa, ameelekeza cha kufanyika. Hili tukio halikuwa la
kufumbia macho,” kilisema chanzo kilichopo ndani ya jeshi la polisi.
POLISI WAPONGEZWA
Wakizungumza
na wanahabari wetu kwa nyakati tofauti, wananchi walilipongeza jeshi la
polisi chini ya Kamanda Kova kwa jinsi walivyolidhibiti kundi hilo.
Abdallah
Juma, mkazi wa Tandale alisema kuwa nguvu ya polisi inapaswa kuungwa
mkono ikiwa ni pamoja na raia kutoa taarifa zinazohusiana na vikundi
kama hivyo.
”Wananchi
tunapaswa kuunga mkono jitihada za jeshi la polisi, tukiungana kwa
pamoja hakika hakutakuwa na wahalifu mitaani na tutaishi kwa raha
mustarehe kuliko siku ile ya Ijumaa usiku,” alisema Abdallah.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
WANASIASA WATAJWA
Chanzo
kilicho ndani ya jeshi la polisi kimewaonya baadhi ya wanasiasa ambao
wanatajwa kuwashinikiza vijana hao kufanya vurugu katika harakati zao za
kisiasa.“Vijana hawahawa wa Panya Road ndiyo wanaotumiwa na baadhi ya
wanasiasa katika mipango yao. Huwa wanawapa fedha na kuwatuma kwenda
kumzomea mgombea fulani, waache mara moja kwani wanachangia kuwapa
nguvu,” kilisema chanzo hicho.
WAJUMBE WA MTAA KUKIONA
Chanzo
kingine kimesema kuwa, mkakati umewekwa kuwataka wajumbe wa serikali za
mitaa jijini Dar kuhakikisha hakuna Panya Road kwenye maeneo yao na
mitaa itakayobainika kuwa na vibaka wengi, wajumbe watawajibishwa.
Comments