Airtel yaitambulisha promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi kwa wakazi wa Arusha

  
 
Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde (katika)  akiongea na wandishi wa habari wakati wa kuitambulisha promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi Mkoani Arusha wakishuhudia Meneja Mauzo kanda ya kaskazini Bwana Brighton Majwala na Afisa Masoko wa Airtel Bi Rebecca Mauma .

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetambulisha promosheni yake ya Airtel yatosha kwa wakazi wa Arusha  na kusisitiza kuwa kila mtanzania ana nafasi ya kujishindia gari Aina ya Toyota IST kila siku.
Akiongea na waandishi wa habari Afisa uhusiano wa Airtel bi Jane Matinde Amesema “tumeona ni vyema kutambulisha  promosheni hii kwa wakazi wa Arusha kwani wao pamoja na watanzania katika mikoa mbalimbali  wananafasi ya kujishindia. Promosheni hii tuliyoizundua rasmi mwanzoni mwa wiki hii inampa nafasi mteja wa Airtel kushiriki na kuingia kwenye droo na kupata nafasi ya kujishindia Toyota IST pindi atakaponunua kifurushi chake chochote cha Airtel yatosha”
Matinde aliongeza kwa kusema ”Mteja atakaponunua kifurushi chake cha siku anaingia kwenye promosheni kwa simu hiyo lakini akinununa cha wiki namba yake itaingia kwenye promosheni kwa muda wa siku saba na akinunua cha mwezi namba yake itaingia kwenye droo kila siku kwa siku thelathini.  Lakini mteja atakaponunua kifurushi chake cha Airtel yatosha cha siku zaidi ya mara moja namba yake itaingia kwenye droo ya siku hiyo kwa idadi ya vifurushi vya siku alivyonunua.
Ili kujiunga na vifurushi vya Airtel yatosha Mteja anatakiwa kupiga *149*99# au kununua vocha ya yatosha au kununua kupitia huduma ya Airtel Money
Huduma ya Airtel yatosha inampa fulsa mtumiaji wa huduma yetu ya Airtel yatosha kupata vifurushi bora na vya bei nafuu sokoni lakini pia inamuwezesha kushinda Toyota IST aliongeza Matinde
Kwa upande wake Meneja Mauzo kanda ya Kaskazini Bwana Brighton Majwala alisema, “promosheni hii ni ya pekee na haina gharama yoyote kujiunga, mteja anapata nafasi ya kushinda kutokana na matumizi yake ya kila siku. 

Wakazi wa Arusha kesho wanapata nafasi ya kuyashuhudia magari haya yakitembea katika mitaa mbalimbali ya jiji la Arusha na tutawapatia wateja wetu nafasi ya kununua line, kujisajili na kupata huduma zetu nyingi na kuwawezesha kujiunga na vifurushi vya yatosha ili waweze kuingia kwenye droo na kupata nafasi ya kujishindia
Hii ni nafasi ya pekee kwako mkazi wa Arusha kuchangamkia zawadi hii nono kwa kujiunga kwenye vifurushi vya yatosha sasa aliongeza Majwala
Airtel yatosha Zaidi ni promosheni yenye lengo la kuwazawadia wateja wake  nchini nzima ambapo kila siku Airtel itatoa Toyota IST moja kwa mshindi wa siku

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.