MWANAMKE mmoja mkazi wa kata ya Ubetu Kahe wilaya ya Rombo mkoani
Kilimanjaro, amefariki dunia baada ya kuuawa na mumewe na kisha mwili
wake kwenye boma la ng’ombe.
Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Geofrey Kamwela amethibitisha
kuuawa kwa mwanamke huyo na kusema tukio hilo limetokea Februari 25
mwaka huu saa 11:45 jion katika nyumba waliyokua wakiishi.
Kamanda amemtaja Mwanamke huyo kuwa ni Jenipher Peter (45) na kuwa
kifo cha mwanamke huyo kinatokana na kipigo alichokipata kutoka kwa
mumewe.
Alisema mwanaume huyo aliyetambuliwa kwa jina la Peter Mrosso (43)
mara baada ya kumuua mkewe alimfukia kwenye boma la kulishia mifugo
mifugo na kisha kumpigia simu jirani akijitapa kuwa amemuua mkewe.
Akielezea tukio hilo, kamanda alisema siku ya tukio jirani wa
familia hiyo alipigiwa simu na Mume wa Marehemu na kumweleza kuwa
amemuua mkewe na kumtelekeza ndani ya Boma la Ng’ombe.
Kamanda alisema taarifa za mauaji ya mwanamke huyo ilitolewa baada ya
Jirani yake kupigiwa simu na Mume wa Marehemu, akimtaarifu kuwa
amemuua mkewe na maiti ameifukia ndani ya Boma la Mifugo.
Alisema baada ya jirani huyo kupewa tarifa hizo, alikwenda kutoa
taarifa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji aitwaye Aloyce Swai (51) na
walipofika eneo la tukio waliukuta mwili wa Marehemu umefukiwa na
udongo na kubakishwa sehemu ya kichwa ikiwa juu.
Baada ya mwili wa Marehemu huyo kufukuliwa ulikutwa ukiwa na majeraha
sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani na Puani na kwamba
baada ya mtuhumiwa kufanya unyama huo alitokomea kusiko julikana .
Kamanda alisema chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika, na kwamba
jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi pamoja na kumsaka mtuhumiwa,
ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa .
Kilimanjaro, amefariki dunia baada ya kuuawa na mumewe na kisha mwili
wake kwenye boma la ng’ombe.
Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Geofrey Kamwela amethibitisha
kuuawa kwa mwanamke huyo na kusema tukio hilo limetokea Februari 25
mwaka huu saa 11:45 jion katika nyumba waliyokua wakiishi.
Kamanda amemtaja Mwanamke huyo kuwa ni Jenipher Peter (45) na kuwa
kifo cha mwanamke huyo kinatokana na kipigo alichokipata kutoka kwa
mumewe.
Alisema mwanaume huyo aliyetambuliwa kwa jina la Peter Mrosso (43)
mara baada ya kumuua mkewe alimfukia kwenye boma la kulishia mifugo
mifugo na kisha kumpigia simu jirani akijitapa kuwa amemuua mkewe.
Akielezea tukio hilo, kamanda alisema siku ya tukio jirani wa
familia hiyo alipigiwa simu na Mume wa Marehemu na kumweleza kuwa
amemuua mkewe na kumtelekeza ndani ya Boma la Ng’ombe.
Kamanda alisema taarifa za mauaji ya mwanamke huyo ilitolewa baada ya
Jirani yake kupigiwa simu na Mume wa Marehemu, akimtaarifu kuwa
amemuua mkewe na maiti ameifukia ndani ya Boma la Mifugo.
Alisema baada ya jirani huyo kupewa tarifa hizo, alikwenda kutoa
taarifa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji aitwaye Aloyce Swai (51) na
walipofika eneo la tukio waliukuta mwili wa Marehemu umefukiwa na
udongo na kubakishwa sehemu ya kichwa ikiwa juu.
Baada ya mwili wa Marehemu huyo kufukuliwa ulikutwa ukiwa na majeraha
sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani na Puani na kwamba
baada ya mtuhumiwa kufanya unyama huo alitokomea kusiko julikana .
Kamanda alisema chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika, na kwamba
jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi pamoja na kumsaka mtuhumiwa,
ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa .
Comments