Wikiendi
iliyopita staa wa sinema za Kibongo, Jacob Steven 'JB' alijikuta
akiangua kilio na kuungwa mkono na mastaa wenzake, Amri Athumani 'Mzee
Majuto' na Single Mtambalike 'Richie' walipomtembelea wodini mama mzazi
wa mtoto Albino, Yohana Bahati (1) aliyeuawa kikatili, Ester Thomas (30)
ambaye naye alijeruhiwa vibaya kichwani, Ijumaa Wikienda
linakuhabarisha.
Tukio
hilo la majonzi lilijiri kwenye Hospitali ya Bugando mkoani hapa ambapo
wasanii hao walikwenda kumfariji mama wa mtoto huyo aliyetekwa mjini
Geita hivi karibuni.
Walipofika
wodini hapo, JB na wenzake walitoa yao ya moyoni kupinga vikali ukatili
aliotendewa mama huyo na mwanaye huku wakitahadharisha juu ya laana
inayoweza kuikumba jamii yetu kwa tukio hilo.
JB: Nampa pole sana mama Yohana. Hii ni aibu kubwa kwa taifa letu na jamii pana duniani.
Watu hawafanyi kazi kujipatia kipato halali. Mafisadi wanataka kujipatia fedha kupitia njia za kishetani za kuwaua wenzetu. Albino ni wenzetu na tunawapenda. Lazima wahalifu wakamatwe na wahukumiwe kunyongwa.
Watu hawafanyi kazi kujipatia kipato halali. Mafisadi wanataka kujipatia fedha kupitia njia za kishetani za kuwaua wenzetu. Albino ni wenzetu na tunawapenda. Lazima wahalifu wakamatwe na wahukumiwe kunyongwa.
Mzee Majuto: Inasikitisha sana. Haivumiliki. Albino ni wenzetu na wana uwezo mkubwa wa kulisaidia taifa letu. Wahusila lazima wakamatwe na tuone wakichukuliwa hatua kali.Richie: Natokwa na machozi. Hiki ni nini? Hatuwezi kufumbia macho jambo hili hasa sisi wenye nafasi kubwa ya kukemea vitendo hivi.Mara baada ya mastaa hao kutoa la moyoni katika wodi aliyolazwa mama huyo, iligeuka kama msiba kwani kila aliyekuwepo alikuwa akiangua kilio kwa uchungu.
Tayari mtoto Bahati amezikwa baada ya mwili wake kupatikana ukiwa hauna baadhi ya viungo huku mama yake akiendelea na matibabu baada ya kufanyiwa oparesheni sehemu ya kichwani aliyojeruhiwa vibaya wakati akinyang'anywa mwanaye.
Tunampa pole sana mama Yohana Bahati, watanzania tuungane kupinga ukatili huu.
Comments