Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiirekebisha tai ya mtoto Amani
Mwinyimvua(11) muda mfupi baada ya kumwapisha Baba yake Hamis Mwinyimvua kuwa
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha katika hafla iliyofanyika ikulu jijini Dar es
Salaam leo asubuhi
Balozi mpya wa Tanzania nchini Kenya Bwana John Haule akila kiapo
mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo.
Balozi mpya wa Tanzania nchini Kenya Bwana John Haule akipeana
mkono na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mara baara ya kula kiapo Ikulu jijini
Dar es salaam leo.
Naibu Katibu mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Hamisi Mwinyimvua akila
kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es
Salaam leo.Picha na Freddy Maro-IKULU
---
---
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amewaapisha Balozi mpya wa
Tanzania nchini Kenya na Naibu Katibu mkuu wa Wizara ya Fedha. Katika hafla
hiyo iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Kikwete amemwapisha Bwana
John Haule kuwa balozi mpya wa Tanzania nchini Kenya na Dkt.Hamisi Mwinyimvua
ameapishwa kuwa naibu katibu mkuu wa Wizara ya Fedha.
Comments