Makamu Mkuu wa chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika Dkt. Tumaini Katunzi akizungumza na wasimamizi na wadadisi wa Sensa ya Viwanda itakayofanyika nchi nzima kuanzia Februari 23 mwaka huu jana jijini Dar es salaam wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi hao.
Baadhi ya wadadisi wa Sensa ya Viwanda wakisaini fomu za viapo vyao mbele ya Kamishna wa Viapo Bw. Oscar Mangula (hayupo pichani) jana jijini Dar es salaam mara baada ya kuhitimu mafunzo ukusanyaji wa takwimu za Sensa ya Viwanda 2013 itakayofanyika Februari 23 mwaka huu.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akifunga rasmi mafunzo ya siku 14 ya wasimamizi na wadadisi wa Sensa ya viwanda 2013 itakayofanyika nchini nzima kuanzia Februari 23,2015. Hafla ya kufunga mafunzo hayo ilifanyika jana eneo la Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika jijini Dar es salaam.
Wadadisi wa Sensa ya Viwanda 2013 wakiapa mbele ya Kamishna wa Viapo Bw. Oscar Mangula (hayupo pichani) jana jijini Dar es salaam mara baada ya kuhitimu mafunzo ya siku 14 ya kuwajengea uwezo wa ukusanyaji wa takwimu za Sensa ya Viwanda 2013 itakayofanyika nchi nzima kuanzia Februari 23 mwaka huu.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akifunga rasmi mafunzo ya siku 14 ya wasimamizi na wadadisi wa Sensa ya viwanda 2013 itakayofanyika nchini nzima kuanzia Februari 23,2015. Hafla ya kufunga mafunzo hayo ilifanyika jana eneo la Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika jijini Dar es salaam.
Comments