- Get link
- Other Apps
Hii bado
ni habari ambayo imeendelea kukaa kwenye headlines....Siku chache
zimepita tangu Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe aanguke kwenye ngazi
akiwa anashuka baada ya kuhutubia wananchi na wanachama wake.Story
ziliendelea mitandaoni kuijadili ishu hiyo, watu wa graphics nao
wakatengeneza picha mbalimbali za kuchekesha kitu ambacho kiliwakwaza
viongozi wa chama cha ZANU-PF.
Leo
vyombo vya habari Zimbabwe vimeripoti kuhusu Rais huyo kuwatimua kazi
wafanyakazi 27 kwenye kikosi cha Usalama kwa kushindwa kuwajibika wakati
Rais huyo akianguka.
Uzembe
ambao unaonekana kufanywa na jamaa hao ni kitendo cha kushindwa kumdaka
kiongozi huyo wakati akianguka, kibaya zaidi ni kwamba alianguka mpaka
chini bila msaada wowote kutoka kwao huku wakiwa wamesimama pembeni
yake.
Vingine
ambavyo huenda hutukuwahi kuvisikia kuhusu ishu hii ni kwamba waandishi
waliopiga picha wakati Rais huyo akianguka walilazimishwa na walinzi wa
Rais kufuta picha hizo.
Taarifa
za kutoka Ikulu ya Rais huyo zinasema huu ni mwanzo tu, uchunguzi
unaendelea na wakipatikana wazembe wengine nao watawajibishwa kama
walivyofanyiwa hapa.
Comments