MISS UNIVERSE NALE BONIFACE ATEMBELEA KITUO CHA WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI (ALBINO) CHA SALVATION ARMY JIJINI DAR ES SALAAM
Miss
Universe Tanzania 2014-2015 Nale Boniface akikabidhi keki kwa
wanafunzi wenye matatizo ya Ngozi (ALBINO) wakati alipotembelea kituo
cha kulelea watoto wenye mahitaji cha Salvatrion Arm jijini Dar es
Salaam ikiwa ni madhimisho ya siku yake ya kuzaliwa ambapo aliamua
kuwapelekea zawadi watoto hao.
Miss
Universe Tanzania 2014-2015 Nale Boniface akikata keki na wanafunzi
wenye matatizo ya Ngozi (ALBINO) wakati alipotembelea kituo cha kulelea
watoto wenye mahitaji cha Salvatrion Arm jijini Dar es Salaam ikiwa ni
madhimisho ya siku yake ya kuzaliwa ambapo aliamua kuwapelekea zawadi
watoto hao.
Miss
Universe Tanzania 2014-2015 Nale Boniface akigawa madaftari kwa
wanafunzi wenye mahitaji wakati alipotembelea kituo cha kulelea watoto
wenye mahitaji cha Salvatrion Arm jijini Dar es Salaam ikiwa ni
madhimisho ya siku yake ya kuzaliwa ambapo aliamua kuwapelekea zawadi
watoto hao.
Miss
Universe Tanzania 2014-2015 Nale Boniface akiwalisha Keki na wanafunzi
wenye matatizo ya Ngozi (ALBINO) wakati alipotembelea kituo cha kulelea
watoto wenye mahitaji cha Salvatrion Arm jijini Dar es Salaam ikiwa ni
madhimisho ya siku yake ya kuzaliwa ambapo aliamua kuwapelekea zawadi
watoto hao.
Sehemu
ya wanafunzi wa kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji cha Salvatrion
Arm jijini Dar es Salaam ikiwa ni madhimisho ya siku yake ya kuzaliwa
ambapo aliamua kuwapelekea zawadi watoto hao.
Feb
26
Muonekano wa Jengo la "Rest House" ya
Magereza Mkoani Morogoro ambalo limezinduliwa rasmi na
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil. kukamilika kwa jengo hilo kutaondoa usumbufu
wa kutafuta hoteli kwa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wanapokuwa safari za kikazi Mkoani Morogoro na pia kuipunguzia
gharama Serikali.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil(suti nyeusi) akijiandaa kukata utepe kwenye
hafla ya Ufunguzi wa Jengo la "Rest House" ya Magereza leo februari 25,
2015 Mkoani Morogoro ambapo ukarabati wa Jengo hilo umefanyika chini ya
Kikosi cha ujenzi cha Jeshi la Magereza(kulia) ni Kamishna Jenerali wa
Jeshi la Magereza, John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja(kushoto) akiwa na
Katibu
Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil akisoma jiwe la
msingi mara baada ya ufunguzi wa Jengo la "Rest House"
ya Magereza leo februari 25, 2015 Mkoani Morogoro.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Mbarak Abdulwakil
akiangalia vyumba mbalimbali vya kulala Maafisa Waandamizi wa Jeshi la
Magereza vilivyopo katika Jengo la "Rest House" ya Magereza, Mkoani
Morogoro(kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir
Minja(kushoto) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt.
Juma Malewa.
Feb
26
Makamu Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Iddi Ramadhani Mapuri akitoa neno la shukrani kwa Mhe.
Waziri wakati wa kikao chake na viongozi wa Tume.
Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Bahame Tom Nyanduga akieleza
mipango ya Tume katika kipindi kijacho wakati wa kikao hicho kabla ya
kumkaribisha Mhe. Waziri kuongea na viongozi wa Tume.
Katibu Mtendaji wa THBUB, Bibi Mary Massay akitoa
taarifa fupi kuhusu utekelezaji wa shughuli za Tume kwa Mhe. Waziri
na ujumbe wake wakati wa kikao hicho.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro akiongea katika kikao chake
na viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), alipotembelea
taasisi hiyo jana (Februari 24, 2015). Kushoto ni Naibu Waziri wa Katiba
na Sheria, Mhe. Ummy Mwalimu na Kulia ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Mhe.
Bahame Tom Nyanduga.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro
na Naibu wake, Mhe. Ummy Mwalimu wakiongea na Mwenyekiti wa THBUB, Mhe.
Bahame Tom Nyanduga ofisini kwake mara baada ya kuwasili katika taasisi
hiyo.
Feb
26
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Push Mobile, Freddie Manento kwa pamoja wakionyesha
ujumbe mfupi wa maneno unaotoa elimu ya ugonjwa wa ebola kwa baadhi ya
wageni waalikwa na waandishi wa habari (hawapo pichani) waliohudhuria
hafla hiyo
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati)
na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Push Mobile, Freddie Manento (kushoto)
wakitiliana saini makubaliano ya ushirikiano wa kukabiliana na ugonjwa
wa ebola kwa kutoa elimu kwa jamii kupitia ujumbe mfupi maneno katika
hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za Mratibu mkazi wa mashirika ya
Umoja wa Mataifa jijini Dar. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mwakilishi wa
UNICEF Tanzania, Dkt. Jama Gulaid.Picha na Umoja wa Mataifa).
Feb
26
Waziri
wa Afrika Mashariki Mhe. Harrison Mwakyembe ambaye alikua mwenyekiti wa
mkutano wa kujiandaa kutiliana saini makubaliano ya biashara na
uwekezaji wa nchi za Afrika Mashariki na Marekani. Utiliano saini huo
utafanyika siku ya Alhamisi Februari 26, 2015 katika Ofisi za Wizara ya
Biashara Marekani, kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,
Balozi Dkt. Richard Sezibera kutoka Burundi.
Ujumbe wa Tanzania
Ujumbe wa Burundi
Ujumbe wa Kenya
Ujumbe wa Uganda na Rwanda
Mkutano ukiendelea.
Balozi
wa Tanzania nchini Martekani akiwa katika picha ya pamoja na Katibu
Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Richard Sezibera kutoka
Burundi.
---
---
Mkutano
uliowakutanisha Mawaziri wa nchi tano za Afrika Mashariki wakiwemo
Mabalozi wa nchini zao nchini Marekani ulifanyika leo siku ya Jumatano
Februari 25, 2015 katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, mkutano
huo uliohusiana na maandalizi ya kutiliana saini ya makubaliano ya
ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kati ya nchi ya Marekani na nchi
za Afrika Mashariki ambazo ni Burundi, Rwanda, Uganda, Kenya na
Tanzania.
Feb
26
kutokana
na Maombi ya mashabiki wengi vijana wa Yamoto Band wameamua kufanya
show moja na ya mwisho nchini Uingereza basi kama ulikosa ile ya London
hii itakuwa si ya kukosa vijana kama kawaida yao wameahidi kufanya vitu
fulani amazingg siku hiyo
DATE:
Saturday 28th February 2015
VENUE:
Kitty Oshea's (Nest to pure gym)
St. peter's Way
Northampton NN1 !PS
Feb
25
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Saalm wawasili katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka Zambia na kupokewa
na mwenyeji wao Rais Edgar Lungu wa Zambia leo asubuhi kwa ziara ya
kikazi ya siku mbili
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma wawasili katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka Zambia na kupokewa
na mwenyeji wao Rais Edgar Lungu wa Zambia leo asubuhi kwa ziara ya
kikazi ya siku mbili
Rais Kikwete na Rais Lungu wa Zambia wakipokea heshima ya mizinga 21 mara baada ya kuwasili.Picha na Freddy Maro-IKULU
Feb
25
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizindua Uborereshaji wa Daftari kla Kudumu la Wapigakura katika mji
mdogo wa Makambako Februari 24, 2015.Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva na Katikati ni Katibu wa Tume
hiyo, Ndugu Malaba.
Baadhi ya watalaamu wa kuandikisha
wapiga wakiwa na zana za kazi kabla ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ya
kuzindua Uborereshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura katika mji
mdogo wa Makambako Februari 24, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akitazama kazi ya uandiskishaji wapiga kura baada ya ya kuzinua
Uborereshaji wa Daftari kla Kudumu la Wapigakura katika mji mdogo wa
Makambako Februari 24, 2015.
Baadhi ya watu waliohudhuria
katika Uzinduzi wa Uborereshaji wa Daftari kla Kudumu la Wapigakura
katika mji mdogo wa Makambako wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
wakati alipohutubia katika uzinduzi huo Februari 24, 2015
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
akizungumza na Mwenyekititi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian
Lubuva (kushpoto) , Naibu Katibu Mkuu na Katibu Mwenezi wa CHADEMA,
John Mnyika (kulia), Yusufu Mbungiro ambaye ni Afisa Uchaguzi na Mafunzo
taifa wa Chama cha CUF (wapili kushoto) na Allan Bujo ambaye ni Mkuu wa
Ulinzi wa CHADEMA baada ya kuzinua Uborereshaji wa Daftarila Kudumu la
Wapigakura katika mji mdogo wa Makambako Februari 24, 2015.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Feb
25
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Wilaya
ya Kinondoni Mhe Paul Makonda baada ya kuwasili katika Shule ya
Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam jana tayari kwa
kukagua ujenzi wa maabara na pia kupokea na kugawa vitabu vya
sayansi vilivyochapishwa na Watu wa
Marekani.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua maabara katika Shule
ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam
ambako pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi
vilivyochapishwa na Watu wa Marekani. Wa kwanza
kulia ni Dkt Shukuru Kawambwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
akifuatiwa na mke wa Rais Mama Salma
Kikwete
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma kikwete, Balozi
wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, na viongozi wengine
wakiangalia jinsi somonla sayansi likifundishwa katika darasa la Kidatu cha
pili Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam
ambako pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi
vilivyochapishwa na Watu wa Marekani
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma kikwete, Balozi
wa Marekani nchini Mhe Mark Childress, Dkt Shukuru Kawambwa,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,na viongozi wengine wakisalimia
wanafunzi katika darasa la Kidatu cha pili Shule ya
Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam ambako pia
alipokea na kugawa vitabu vya sayansi
vilivyochapishwa na Watu wa Marekani
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Marekani
nchini Mhe Mark Childress, wakiongea na mkandarasi wa maabara
ya Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e salaam
ambako pia alipokea na kugawa vitabu vya sayansi vilivyotolewa na Watu wa
Marekani
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma Kikwete
na Balozi wa Marekani nchini Mhe Mark Childress wakiwa na baadhi ya
wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja huko Kunduchi jijini Dar e
salaam wakiwa na vitabu vya sayansi vilivyochapishwa na Watu wa
Marekani
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakuja
huko Kunduchi jijini Dar e salaam wakiimba kwa furaha katika
sherehe ya kukabidhiwa vitabu vya sayansi vilivyochapishwa na
Watu wa Marekani
Subscribe to:
Posts (Atom)
Comments