MKUU WA MKOA WA RUKWA AFUNGA MAFUNZO YA SIKU MBILI YALIYOANDALIWA NA TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA TANZANIA KWA KAMATI ZA MAADILI MIKOA YA RUKWA NA KATAVI LEO
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akisoma hotuba ya kufunga mafunzo
ya siku mbili yaliyoandaliwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama Tanzania
kwa kamati za maadili Mikoa ya Rukwa na Katavi na kufanyika Mjini
Sumbawanga tarehe 12-13 Februari 2015. Katika hotuba yake hiyo ameiomba
Serikali kutenga fedha ya kutosha ili mafunzo kama hayo yaweze kuwafikia
watu wengi zaidi kwa ustawi wa Sheria na Haki nchini.
Mafunzo hayo ni katika mkakati wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Tanzania kuimarisha tume za maadili nchini kusaidia maadili kwa watumishi wa Mahakama nchini. Kushoto ni Jaji Ferdinand Wambali muwezeshaji wa mafunzo hayo ambae ni Jaji wa Mahakama Kuu na Mkuu wa Chuo cha Mahakama Lushoto .
Bi Enzel Mtei ambae ni miongoni mwa wawezeshaji wa mafunzo hayo kutoka Tume
ya Mahakama Tanzania akimuwakilisha Mtendaji Mkuu wa Mahakama
akizungumza muda mfupi kabla ya kuhitimishwa mafunzo hayo. Miongoni mwa
maazimio yaliyofikiwa katika mafunzo hayo kwa wanakamati; Mihimili yote
ya dola nchini ifanye kazi kwa pamoja ili kutoa haki kwa wakati, Amri
halali itakayotolewa namamlaka husika iheshimiwe kuleta usawa wa
kisheria nchini na Mahakimu pamoja na wadau wengine wa sheria wawe mfano
kwa maadili bora katika jamii.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa katikati na wajumbe wengine wakifuatilia mafunzo hayo.
Wajumbe wa Kamati ya maadili Mikoa ya Rukwa na Katavi wakifuatilia mafunzo hayo.
Wajumbe wa Kamati ya maadili Mikoa ya Rukwa na Katavi wakifuatilia mafunzo hayo.
Wajumbe wa Kamati ya maadili Mikoa ya Rukwa na Katavi wakifuatilia mafunzo hayo.(Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa@Rukwareview.blogspot.com)
Comments