MWAKALEBELA AUKWAA UKUU WA WILAYA

IMG_2170
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya wakuu wa wilaya wapya 27 lakini katika idadi hiyo jina la Katibu Mkuu wa zamazi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Fredrick Wilfred Mwakalebela limo ndani yake.
Mwakalebela amepata ulaji huo ambapo sasa anakwenda kuiongoza wilaya ya Wanging’ombe iliyopo Njombe huku mwanahabari Shabani Kissu akipelekwa Kondoa.
Akizungumza na shaffih Dauda Mwakalebela ambaye alikuwa katibu mkuu wa kwanza katika utawala wa Rais Leodgar Tenga amesema ameishukuru serikali kwa kuona mchango wake kwamba anaweza kuisaidia nchi yake.
“Kwanza niishukuru serikali kupitia Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kwa kunioan bado nina mchango wa kuisaidia nchi yangu lakini baada ya hilo nataka kufika katika kibarua changu hicho kujua changamoto zinaziwakabili wananchi wa huko,”alisema Mwakalebela.
“Nikishafanya utambuzi huo sasa nitaanza mikakati ya kuanza utatuzi kwa haraka nikisaidiana na wananchi wa huko, kikubwa naomba ushirikiano kwa wakazi wenzangu wa Wang’ing’ombe.”

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.