RAIS Jakaya Kikwete amefanya
mabadiliko ya wakuu wa wilaya wapya 27 lakini katika idadi hiyo jina la
Katibu Mkuu wa zamazi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Fredrick
Wilfred Mwakalebela limo ndani yake.
Mwakalebela amepata ulaji huo
ambapo sasa anakwenda kuiongoza wilaya ya Wanging’ombe iliyopo Njombe
huku mwanahabari Shabani Kissu akipelekwa Kondoa.
Akizungumza na shaffih Dauda
Mwakalebela ambaye alikuwa katibu mkuu wa kwanza katika utawala wa Rais
Leodgar Tenga amesema ameishukuru serikali kwa kuona mchango wake kwamba
anaweza kuisaidia nchi yake.
“Kwanza niishukuru serikali
kupitia Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kwa kunioan bado nina mchango wa
kuisaidia nchi yangu lakini baada ya hilo nataka kufika katika kibarua
changu hicho kujua changamoto zinaziwakabili wananchi wa huko,”alisema
Mwakalebela.
“Nikishafanya utambuzi huo sasa
nitaanza mikakati ya kuanza utatuzi kwa haraka nikisaidiana na wananchi
wa huko, kikubwa naomba ushirikiano kwa wakazi wenzangu wa
Wang’ing’ombe.”
Comments