Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete (wa pili kutoka
kulia) na mgeni wake Rais wa Shirikisho la Ujerumani, Joachim Gauck (wa
tatu kutoka kulia) wakifurahia wakati wa dhifa ya kitaifa ya chakula cha
usiku aliyomwandalia kiongozi huyo jana usiku, Ikulu jijini Dar es
salaam. Kushoto ni Mke wa Rais wa Tanzania, mama Salma Kikwete na Mke wa
Rais wa Ujerumani Bi. Daniella Schadt.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete(wa pili kutoka
kulia) akiwa na mgeni wake Rais wa Shirikisho la Ujerumani, Joachim
Gauck (wa tatu kutoka kulia) wakiwa wamesimama wakati wimbo taifa wa
Tanzania na ujerumani ulipopigwa wakati wa dhifa ya kitaifa ya chakula
cha usiku aliyomwandalia kiongozi huyo jana usiku, Ikulu jijini Dar es
salaam. Kushoto ni Mke wa Rais wa Tanzania, mama Salma Kikwete na Mke
wa Rais wa Ujerumani Bi. Daniella Schadt.
Baadhi ya viongozi mbalimbali wa Serikali waliohudhuria dhifa hiyo jana usiku, Ikulu jijini Dar es salaam.
Mkuu
wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Askofu Gehazi Malasusa (wa
pili kutoka kushoto) na viongozi wengine wa Serikali wakiwa kwenye dhifa
ya kitaifa ya chakula cha usiku aliyoandaliwa Rais wa Ujerumani Joachim
Schadt na Rais Jakaya Kikwete jana usiku jijini Dar es salaam.
Rais
wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete na mgeni wake Rais wa Shirikisho la
Ujerumani Mh. Joachim Gauck wakielekea sehemu ya nyuma ya ukumbi
kutazama Brass bendi ya Jeshi la Polisi iliyokuwa ikitoa burudani wakati
wa dhifa ya kitaifa ya chakula cha usiku aliyomuandalia mgeni wake jana
usiku Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais
wa Shirikisho la Ujerumani Mh. Joachim Gauck akitoa ujumbe wake kwa
wageni mbalimbali waliohudhuria dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais
Jakaya Kikwete Ikulu.
Rais
wa Ujerumani Mh. Joachim Gauck na Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania
wakitazama vikundi mbalimbali vya ngoma za asili vilivyokuwa
vikitumbuiza wakati wa dhifa ya kitaifa Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais
wa Shirikisho la Ujerumani Mh. Joachim Gauck (wa pili kutoka kulia)
akiteta jambo na Rais mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi jana usiku
wakati wa dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais Jakaya Kikwete Ikulu
jijini Dar es salaam. Kushoto ni mke wa Rais wa Ujerumani Bi. Daniella
Schadt na mama Sitti Mwinyi Mwinyi.
Rais
wa Shirikisho la Ujerumani Mh. Joachim Gauck (wa pili kutoka kulia)
akiteta jambo na Rais mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi jana usiku
wakati wa dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na Rais Jakaya Kikwete Ikulu
jijini Dar es salaam. Kushoto ni mke wa Rais wa Ujerumani Bi. Daniella
Schadt na mama Sitti Mwinyi Mwinyi.
Mkuu
wa wilaya ya Temeke Sophia Mjema (kushoto) akiongea na baadhi ya wageni
waalikwa akiwemo Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Diana Melrose
(aliyesimama) wakati wa dhifa ya kitaifa ya chakula cha usiku
iliyoandaliwa na Rais Jakaya Kikwete kwa Rais wa Ujerumani Mh. Joachim
Gauck , Ikulu jana usiku.
Rais
wa Shirikisho la Ujerumani Mh. Joachim Gauck na Rais Jakaya Kikwete wa
Tanzania wakitazama Brass Bendi ya Jeshi la Polisi iliyokuwa ikitumbuiza
wakati wa dhifa hiyo Ikulu jijini Dar es salaam.
Comments