RAIS Jakaya Kikwete amefanya uteuzi wa wakuu wa wilaya wapya 27 pamoja na
mabadiliko ya vituo vya kazi kwa baadhi ya wakuu wa wilaya wa mwanzo kwa lengo
la kuboresha utendaji Serikalini.
Akitangaza wakuu hao wa wilaya mjini hapa jana ,Waziri Mkuu Mizengo Pinda
alisema kuwa,mabadiliko hayo yamezingatia kuwepo kwa nafasi 27 zilizoachwa wazi
kutokana na sababu mbalimbali.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni kufariki kwa wakuu wa wilaya watatu,wakuu wa
wilaya watano kupandishwa vyeo kuwa wakuu wa mikoa ,wakuu wa wilaya saba
kupangiwa majukumu mengine huku wakuu wilaya 12 wakitenguliwa uteuzi wao.
Alisema katika mchakato huo,wakuu wa wilaya 64 wamebailishwa vituo vya kazi
na wakuu wa wilaya 42 wameendelea katika vituo vyao vya kazi vya awali.
Pinda aliwataja waliwataja wakuu wa wilaya wapya kuwa ni pamoja na Mariam
Mtima (Ruangwa),Dk.Jasmine Tiisike (Mpwapwa),Pololeti Mgema (Nachingwea),Fadhili
Nkurlu (Misenyi),Felix Lyaniva (Rorya),Fredrick Mwakalebela (Wanging'ombe) na
Zainabu Mbussi (Rungwe) .
Francis Mwonga(Bahi),Kiming'ombe Nzoka (Kiteto),Husna Msangi
(Handeni),Emmanuel Uhaula (Tandahimba),Mboni Mhita (Mufindi),Hashim Mgandilwa
(Ngorongoro) ,Mariam Juma (Lushoto),Thea Ntara (Kyela),Ahmad Nammohe (Mbozi) na
Shaaban Kisu ( Kondoa).
Wengine ni Zelothe Steven (Musoma),Pili Moshi (Kwimba),Mahmoud Kambona
(Simanjiro) ,Glorius Luoga (Tarime),Zainabu Telack (Sengerema),Benard Nduta
(Masasi),Zuhura Ally (Uyui) ,Paul Makonda (Kinondoni),Mwajuma Nyiruka (Misungwi)
na Maftah Mohamed (Serengeti).
Vile vile Pinda aliwataja waliotenguliwa uteuzi wao kutokana na sababu
mbalimbali zikiwemo sababu za kiumri ,kiafya kuwa ni pamoja na James Millya
aliyekuwa Mkuu we wilaya ya Longodo,Elias Lali aliyekuwa mkuu wa wilaya ya
Ngorongoro,Alfred Msovella aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kongwa ,Danny Makanga
aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Kasulu,Fatma Kimario aliyekuwa mkuu wa wilaya ya
Kisarawe.
Wengine waliotenguliwa ni Elibariki Kingu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya
Igunga,Dk.Leticia Warioba aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Iringa ,Evaristi Kalalu
aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mufindi,Abiud Saidea aliyekuwa mkuu wa wilaya ya
Momba,Martha Umbulla aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kiteto,Khalid Mandia aliyekuwa
Mkuu wa wilaya ya Babati na Elias Goroi.
Aidha Pinda aliwataja wakuu wa wilaya ambao uteuzi wao umetenguli na
kupangiwa majukumu mengine ni wakuu wa wilaya saba ambao ni Brigedia Generali
Cosmas Kayombo aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Kanali Ngemela Elson
Lubinga aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mlele na Juma Madaha aliyekuwa mkuu wa
wilaya ya Ludewa.
Pia wamo,Mercy Silla aliyekuwa mkuu wa wilaya Mkuranga,Ahmed Kipozi
aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Bagamoyo,Mrisho Gambo aliyekuwa mkuu wa wilaya ya
Korogwe na Elinas Pallangyo aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Rombo.
Kwa mujibu wa Pinda wakuu wa wilaya waliofariki kuwa ni Kaptein Yamungu
aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Serengeti,Anna Magoha aliyekuwa mkuu wa wilaya ya
Urambo na Moshi Chang'a aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kalambo.
Waziri Mkuu Pinda amewataka wakuu wa wilaya waliobadilishwa vituo kuanza
kazi mara moja huku akisema wapya wanasubiri kupatiwa mafunzo ili kuboresha
uwajibikaji wao.
xxxxxxxx
Joyce Kasiki,Dodoma
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema taarifa za Mfuko wa Pensheni wa PSPF
zinaonesha limbikizo la mikopo ya serikali hadi kufikia desemba 2014 ni
sh.bilioni 517.9 huku madeni ya mifuko yote ya hifadhi ya jamii kwa serikali ni
shilingi trilioni 1.8.
Waziri Mkuu Pinda alitoa kauli hiyo wakati akifungua Mkutano wa Nne wa
mwaka wa wadau wa Mfuko huo uliofanyika mjini hapa alisema ,malimbikizo ya
michango ya watumishi wa Serikali hadi hadi ilipofanyika tathmini ya mfuko huo
mwaka 2010 ni sh.Trilioni 4.04.
Pinda alisema, madeni hayo yamekuwa yakiathiri shughuli za mifuko hususan
katika Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na mifuko hiyo.
"Lakini hata hivyo,Serikali imeandaa mkakati wa kuyashughulikia na kuondoa
hofu kuhusu taarifa zilizopo kwamba mifuko hiyo ipo katika hatari ya kufa
kutokana na madeni hayo." alisema Pinda
Alisema , baadhi ya athari za madeni hayo kuwa ni pamoja na kupunguza uwezo
wa mfuko kulipa wanachama kwa wakati,kushindwa kuwekeza kabisa kitu ambacho
hakitatokea kwa sababu serikali, malalamiko kutoka kwa wastaafu kuhusu
kucheleweshwa malipo yao.
"Serikali imeshaanza kulipa sehemu ya deni hilo na taarifa za Hazina
zinaonesha hadi sasa shilingi bilioni 160 zimelipwa kwa upande wa PSPF na
anaelewa changamoto iliyopo ni kasi ndogo ya malipo."
Aidha alibainisha alisema malalamiko ya wanachama wa Mfuko huo ya
kucheleweshewa malipo ya mafao yao yanaweza kupatiwa ufumbuzi na mfuko
huo.
Alisema yapo malalamiko ya wanachama wengi wanaojiunga na mifuko ya hifadhi
ya jamii kwamba upo usumbufu mkubwa katika kupata taarifa sahihi kutoka kwenye
mfuko.
“Upo ucheleweshaji mkubwa katika malipo ya pensheni pale mfanyakazi au
mwanachama anapostaafu , Vile vile lipo tatizo la wanachama kutoridhishwa na
faida ya uwekezaji, Malalamiko haya yanaweza kabisa kupatiwa ufumbuzi,”alisema
Pinda
Hata hivyo alisema takwimu zilizopo zinaonyesha ni asilimia 5.9 tu ya nguvu
kazi ya Watanzania waliopo katika sekta rasmi ndio wanaopata huduma ya hifadhi
ya jamii huku akisema, takwimu hizo ni
kielelezo tosha cha kuonyesha changamoto inayoikabili sekta ya hifadhi ya
jamii.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, alisema changamoto
kubwa inayowakabili ni watumishi ambao wanaokaribia kustaafu kushindwa
kuwasilisha nyaraka muhimu zinazohitajiika ili ziweze kusaidia katika kuandaa
mafao yao kwa wakati.
Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya mfuko wa PSPF,George
Yambesi aliiomba Serikali kuongeza kasi ya ulipaji wa deni la mfuko huo ili
mfuko huo uweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
Waliobadilishwa vituo ni
Nyerembe
Munasa anatoka Arumeru anakwenda Mbeya, Jordan Rugimbana alikuwa Kinondoni
anakwenda Morogoro, Fatma Salum Ally kutoka Chamwino kwenda Mtwara, Lephy Gembe
kutoka Dodoma Mjini kwenda Kilombero na Christopher Kangoye kutoka Mpwapwa
kwenda Arusha.
Wengine ni
Omar Kwaang’ kutoka Kondoa kwenda Karatu, Francis Mtinga kutoka Chemba kwenda
Muleba, Elizabeth Mwasa kutoka Bahi kwenda Dodoma, Agnes Hokororo kutoka Ruangwa
kwenda Namtumbo, Regina Chonjo kutoka Nachingwea kwenda Pangani, Husna Mwilima
kutoka Mbogwe kwenda Arumeru na Gerald Guninita kutoka Kilolo kwenda
Kasulu.
Wengine
waliobadilishwa vituo vya kazi ni Zipora Pangani kutoka Bukoba kwenda Igunga,
Kanali Issa Njiku kutoka Misenyi kwenda Melele, Richard Mbeho kutoka Biharamuro
kwenda Momba, Lembris Kipuyo kutoka Muleba kwenda Rombo, Ramadhani Maneno kutoka
Kigoma kwenda Chemba, Venance Mwamoto kutoka Kibondo kwenda Kaliua, Gishuli
Charles kutoka Buhigwe kwenda Ikungi, Novatus Makunga kutoka Hai kwenda Moshi na
Anatory Choya kutoka Mbulu kwenda Ludewa.
Wengine ni
Christine Mndeme kutoka Hanang’ kwenda Ulanga, Jackson Musome kutoka Musoma
kwenda Bukobna, John Henjewele kutoka Tarime kwenda Kilosa, Dk Norman Sigalla
kutoka Mbeya kwenda Songea, Dk Michael Kadeghe kutoka Mbozi kwenda Mbulu, Cripin
Meela kutoka Rungwe kwenda Babati na Magreth Malenga kutoka Kyela kwenda
Nyasa.
Said Amanzi kutoka Morogoro kwenda
Singida,Antony Mtaka kutoka Mvomero kwenda Hai, Elias Tarimo kutoka Kilosa
kwenda Biharamulo, Francis Miti kutoka Ulanga kwenda Hanang’, Hassan Masala
kutoka Kilombero kwenda Kibondo, Angelina Mabula kutoka Butiama kwenda Iringa,
Farida Mgomi Kutoka Masasi kwenda Chamwino, Wilman Ndile kutoka Mtwara kwenda
Kalambo.
Ponsian Nyami kutoka Tandahimba
kwenda Bariadi,Mariam Lugaila kutoka Misungwi kwenda Mbogwe, Mary Onesmo kutoka
Ukerewe kwenda Buhigwe, Karen Yunus kutoka Sengerema kwenda Magu, Josephine
Matiro kutoka Makete kwenda Shinyanga, Joseph Mkirikiti kutoka Songea kwenda
Ukerewe, Abdula Lutavi kutoka Namtumbo kwenda Tanga, Ernest Kahindi kutoka Nyasa
kwenda Longido, Anna Nyamubi kutoka Shinyanga kwenda Butiama na Rosemary
Kirigini kutoka Meatu kwenda Maswa.
Abdalla Ali Kihato kutoka Maswa
kwenda Mkuranga, Erasto Sima kutoka Bariadi kwenda Meatu, Queen Mulozi kutoka
Singida kwenda Ulambo, Yahaya Nawanda kutoka Iramba kwenda Lindi, Manju Msambya
kutoka Ikungi kwenda Ilemela, Saveli Maketta kutoka Kaliua kwenda Kigoma, Bituni
Msangi kutoka Nzega kwenda Kongwa na Lucy Mayenga kutoka Uyui kwenda
Iramba.
Majid Mwanga kutoka Lushoto kwenda
Bagamoyo, Muhingo Rweyemamu kutoka Handeni kwenda Makete, Hafsa Mtasiwa kutoka
Pangani kwenda Korogwe, Dk Nassor Ali Hamid kutoka Lindi kwenda Mafia, Festo
Kiswaga kutoka Nanyumbu kwenda Mvomero, Sauda Mtondoo kutoka Mafia kwenda
Nanyumbu, Seleman Mzee kutoka Kwimba kwenda Kilolo, Ertirina Kilasi kutoka
Wanging’ombe kwenda Muheza, Subira Mgalu kutoka Muheza kwenda Karagwe na
Jacqueline Liana kutoka Magu kwenda Nzega.
Wanaobaki katika vituo vyao vya kazi
Wakuu wa wilaya wanaobaki katika
vituo vyao ni Jowika Kasunga (Monduli), Raymond Mushi (Ilala), Sophia Mjema
(Temeke), Amani Mwenegoha (Bukombe), Ibrahimu Marwa (Nywang’wale), Rodrick
Mpogolo (Chato) Manzie Mangochie (Geita), Darry Rwegasira (Karagwe), Luteni
Kanali Bnedict Kitenga (Kyerwa) na Constatine Kanyasu (Ngara).
Wengine ni Paza Mwamulima (Mpanda),
Peter Kiroya (Kakonko), Hadija Nyembo (Uvinza), Dk Charles Mlingwa (Siha),
Shaibu Ndemanga (Mwanga), Herman Kapufi (Same), Ephraimu Mbaga (Liwale),
Abdallah Ulega (Kilwa), Joshua Mirumbe (Bunda), Deodatus Kinawiro (Chunya),
Rosemary Senyamule (Ileje) na Galamhusein Shaban (Mbarali).
Wengine waliobaki ni Christopher
Mgala (Newala), Barika Konisaga (Nyamagana), Sara Dumba (Njombe), Hanifa
Karamagi (Gairo), Halima Kihemba (Kibaha), Nurdin Babu (Rufiji), Methew Sedoyeka
(Sumbawanga), Idd Kimanta (Nkasi), Chande Nalicho (Tunduru)), Senyi Ngaga
(Mbinga), Wilson Nkambaku (Kishapu) na Benson Mpesya (Kahama).
Wengine ni Paul Mzindakaya (Busega),
Georgina Bundala (Itilima), Fatma Toufiq (Manyoni), Luten Edward Ole Lenga
(Mkalama), Hanifa Selengu (Sikonge), Seleman Kumchaya (Tabora), Mboni Mgaza
(Mkinga na Seleman Liwowa (Kilindi).
Waliopandishwa cheo ni John Mongela
aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Arusha amekuwa mkuu wa mkoa wa Kagera,Amina MAsenza
aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Ilemela amekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa,Dk.Ibrahim
Khamis aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Moshi amekuwa mkuu wa mkoa wa katavi ,Halima
Dendego aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Tanga
amekuwa mkuu wa mkoa wa Mtwara na Daud Ntibenda aliyekuwa mkuu wa wilaya amekuwa
mkuu wa mkoa wa Arusha.
Comments