Mwenyekiti wa Kamati ya Kuratibu maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama (kulia) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, ambapo alielezea ujio wa wasanii wa muziki wa injili kutoka nchi za Afrika Kusini, Zambia,Malawi, Rwanda, Kenya na Burundi.
Pia alielezea jinsi tamasha hilo lilivyosaidia kusomesha watoto yatima 350 na kutoa misaada mbalimbali ya vyakula na vifaa kwa vituo vya kulelea wanaoishi kwenye mazingira magumu ambapo wajane wamepatiwa mitaji yenye yenye thamani ya sh. mil. 79.
Amesema kuwa kuwa kwa vile Tamasha la Pasaka lipo kwa watu wasiojiweza, kamati imeamua kujenga Kituo Kikubwa nchini cha kutolea misaada mbalimbali kwa ajili ya watu hao
Pia alikemea mauaji ya Albino yanayoendelea nchini, ambapo ameishauri serikali kkuwakusanya watoto alibino na kuwaweka sehemu moja ambayo watapata huduma ya ulinzi na malazi hadi watakapokuwa ndipo waruhusiwe kutoka katika kambi hiyo.
Pia aliwaasa viongozi wa siasa kuacha tabia za kishirikina ya kushawishika kutumia vioungo vya albino kwa lengo la kupata vyeo.
.Tamasha hilo linatarajia kufanyika Aprili 5,mwaka huu. Kushoto ni mmoja wa Wajumbe wa kamati hiyo, Khamis Pembe. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Pia alielezea jinsi tamasha hilo lilivyosaidia kusomesha watoto yatima 350 na kutoa misaada mbalimbali ya vyakula na vifaa kwa vituo vya kulelea wanaoishi kwenye mazingira magumu ambapo wajane wamepatiwa mitaji yenye yenye thamani ya sh. mil. 79.
Amesema kuwa kuwa kwa vile Tamasha la Pasaka lipo kwa watu wasiojiweza, kamati imeamua kujenga Kituo Kikubwa nchini cha kutolea misaada mbalimbali kwa ajili ya watu hao
Pia alikemea mauaji ya Albino yanayoendelea nchini, ambapo ameishauri serikali kkuwakusanya watoto alibino na kuwaweka sehemu moja ambayo watapata huduma ya ulinzi na malazi hadi watakapokuwa ndipo waruhusiwe kutoka katika kambi hiyo.
Pia aliwaasa viongozi wa siasa kuacha tabia za kishirikina ya kushawishika kutumia vioungo vya albino kwa lengo la kupata vyeo.
.Tamasha hilo linatarajia kufanyika Aprili 5,mwaka huu. Kushoto ni mmoja wa Wajumbe wa kamati hiyo, Khamis Pembe. (PICHA NA RICHARD MWAIKENDA)
Comments