WAKILI: MAHAKAMA IMEMTENDEA HAKI MACHA


NA MWANDISHI WETU
UPANDE wa utetezi katika kesi iliyokuwa ikimkabili mfanyabiashara Hans Macha, umesema Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imetenda haki kwa kuthibitisha kuwa mteja wao alinunua nyumba kihalali kutoka kwa mlalamikaji Ramadhani Balenga.

Kauli hiyo ya upande wa utetezi, imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Devotha Kisoka kutoa hukumu iliyothibitisha kwamba Macha alinunua nyumba kihalali kutoka kwa Balenga.

Wakili wa Macha, Deo Ringia alidai mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam, kwamba mahakama hiyo imetenda haki kwa sababu ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri ulikuwa na mashaka na wa kuunga unga.

Alidai kwa upande wao, wamepokea hukumu hiyo kwa furaha zaidi kwani haki imetendeka.

"Haki imetendeka na mteja wetu amepumua. Tumeipokea hukumu kwa furaha zaidi kwani haki imetendeka kwa sababu hata usahahidi wa upande wa Jamhuri ulivyokwenda ulikuwa na mashaka na wa kuunga unga," alidai.

Wakili Ringia alidai atazungumzia zaidi hukumu hiyo ambayo Hakimu Moshi aliisoma kwa kifupi, baada ya kupata nakala yake.

Novemba, mwaka jana, mahakama hiyo ilimuona Macha ana kesi ya kujibu na kutakiwa kuwasilisha utetezi wake, baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wake.

Macha wakati akijitetea aliita mashahidi takriban 10 ambapo, alikanusha tuhuma hizo kwa madai ni za uongo na kuiomba mahakama kuyatupilia mbali mashitaka hayo.

Alidai tuhuma hizo ni za uongo kwa sababu Balenga anafahamu kwamba alimuuzia nyumba hiyo. --

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.