WAZIRI MKUU PINDA KUFANYA ZIARA YA KIKAZI MKOANI MBEYA.


Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro





WAZIRI mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mizengo Pinda,anatarajia
kufanya ziara ya ya kikazi kwa siku nane mkoani Mbeya.



Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abass Kandoro,alisema jana(Feb 20) kuwa Pinda
anatarajiwa kuwasili mkoani hapa Februari 23 majira ya saa kumi jioni na
akiwa mkoani hapa atatembelea halmashauri saba.



Kandoro alizitaja halmashauri zitakazotembelewa na waziri mkuu kuwa ni
halmashauri ya wilaya ya Mbeya,jiji la Mbeya,Kyela,Busokelo,Rungwe,Chunya
na Mbozi.



Alisema lengo la ziara hiyo ni kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo
inayotekelezwa na serikali,halmashauri na wadau mbalimbali wa maendeleo
katika mkoa wa Mbeya.



Mkuu huyo wa mkoa alisema katika ziara yake,Pinda atakagua,kuweka mawe ya
msingi na kuzindua miradi latika sekta ya Elimu,Afya,ujenzi,barabara,kilimo
na umwagiliaji,maji,masoko na hifadhi ya chakula.



Alisema pia waziri mkuu akiwa katika halmashauri hizo atahutubia wananchi
katika mikutano ya hadhara hivyo aliwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi
kwenye mikutano hiyo sambamba na maeneo mengine atakayopitia.
Na Mbeya yetu

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*