Waziri Pinda : Tutaunganisha nguvu kwa mgombea urais atakayeteuliwa na chama

                 

IMG_4287
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwahutubia wananchi wa tarafa ya Pawaga
IMG_4281
Waziri Mkuu Pinda akiwapungia mikono wananchi wa tarafa ya Pawaga
IMG_4280
Wananchi wa tarafa ya Pawaga wakimshangilia Waziri Mkuu Pinda
IMG_4249
Wananchi wa tarafa ya Pawaga, Iringa wakimsikiiza Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewataka watanzania hasa wana Chama wa cha Mapinduzi ( CCM) kuwa na subira katika kumpata mwanachama atakayefaa kusimama kugombea urais kupitia CCM mwaka huu.
Kuwa tayari wengi sana wamejitangaza wazi wazi na wengine wamejitangaza kimya kimya kutaka kugombea Urais na kuwa yote heri ila chama kina utaratibu wake.
" Itafika wakati ambao kila chama kitasema huyu ndie mtu wetu ambae atapambana na vyama vingine ...tunachosema sisi huyo atakayependekezwa ndie atakuwa mgombea wetu"alisema Waziri Pinda
Waziri Pinda alitoa kauli hiyo leo wakati akiwahutubia wakazi wa tarafa ya Pawaga Baada ya kuzindua skimu ya umwagiliji itakayowanufaisha wakazi wa vijiji vitatu kikiwemo cha Magozi, Ilolompya na Mkombilenga uliogharimu zaidi ya Tsh bilioni 1.6 fedha kutoka kwa wahisani na serikali.
Alisema kuwa utaratibu wa ndani ya chama anbacho wao ni watawala na wanaoendelea kuyafanya maendeleo yanaonekana watalazimika kumuunga mkono atakayeteuliwa na wale wote ambao hawajateuliwa watamuunga mkono atakayeteuliwa kwa makundi yote kuvunjwa na kuwa na Kundi moja pekee.
Kuwa baada ya mgombea wa chama tawala kupatikana jukumu kubwa ni kuwaomba wapenzi wao wote kumchagua huyo aliyeteuliwa na chama.
Hivyo Waziri Pinda aliwataka wananchi kote nchini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga Kura.
Alisema kuwa zoezi hilo ambalo litawahusu wale wote wenye miaka kuanzia 18 na kuendelea linatarajia kuanza mwezi huu katika Mkoa wa Njombe na kuwa kila kata zoezi hilo litadumu kwa muda wa wiki mbili ama tatu .
"Nawaombeni kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na pia kuipigia kura katiba inayopendekezwa muda ukifika sisi tunaamini ni katiba bora ambayo imegusa makundi yote yakiwemo ya wafugaji na wakulima pamoja na makundi mengine"
Kuwa wapo wapotoshaji ambao watafika na kuwadanganya juu ya katiba hiyo inayopendekezwa na wasiwasikilize.
Alisema kazi kubwa imefanyika katika kuandaa katiba hiyo inayopendekezwa mbali ya wao (UKAWA) kutoka nje wakati wa bunge hilo la katiba lakini wajumbe waliobaki walifanya kazi nzuri ya kuandaa katiba hiyo inayopendekezwa hivyo kuwaomba wananchi kuipigia kura.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Pinda amewataka wakulima wa Mpunga Pawaga katika kuepuka na migogoro kati yao na wafugaji kuweka utaratibu wa kukusanya majani ya Mpunga na kuyapeleka majumbani kwao ili wafugaji wapate kununua kuliko kuyaacha mashambani na kuwafanya wafugaji kuingiza mifugo yao mashambani.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*