Wizara ya Nishati na Madini imepata Tuzo ya Ki­mataifa ya mwaka ya Maende­leo ya Udhibiti wa Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi.


Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene (kulia)  akipokea Tuzo ya Ki­mataifa ya mwaka ya Maende­leo ya Udhibiti wa Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi inayotolewa na Kampuni ya Kimataifa ya Wildcat International, ya nchini Marekani kupitia machapisho yake maarufu Duniani ya The Oil & Gas Year (TO&GY). Anayemkabidhi Tuzo hiyo ni Mratibu wa Mahusiano kwa Wateja kutoka Jarida la TO&GY, Bi. Laura Carr.
----
Na Teresia Mhagama

Wizara ya Nishati na Madini imepata Tuzo ya Ki­mataifa ya mwaka ya Maende­leo ya Udhibiti wa Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi.

Tuzo hiyo ya mwaka 2014 inayotolewa na Kampuni ya Kimataifa ya Wildcat International, ya nchini Marekani kupitia machapisho yake maarufu Duniani ya The Oil & Gas Year (TO&GY), imekabidhiwa rasmi jijini Dar es Salaam kwa Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene ambaye alipokea Tuzo hiyo kwa niaba ya Wizara.

Tuzo hiyo, iliyotolewa na Mratibu wa Mahusiano kwa Wateja kutoka Jarida la TO&GY, Bi. Laura Carr inaitambua Wizara  kutokana na mafan­ikio yake katika kushughulikia changamoto za udhibiti wa sekta ndogo ya mafuta na gesi na hivyo kuchochea maende­leo ya sekta hiyo.

Mafanikio hayo ni pamoja na kuwa na sera mpya ya gesi asilia,  kuwa na muundo mpya wa makubaliano ya gharama za utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi (Production- Sharing Agreement), na kuwa na Rasimu ya Sera Uweze­shaji na Ushirikishaji Wazawa (local content policy).

“Hayo ni baadhi tu ya maendeleo yaliyofanya sekta hii kueleweka na kuku­balika zaidi kwa wawekezaji na wadau,” imesema sehemu ya Jarida la TO&GY.

Pamoja na Tuzo ya Wiz­ara ya T0&GY, Shirika la Umeme nchini kupitia Mkurugenzi wake, Mhandisi Felchesmi Mramba ameshinda Tuzo ya Mtu wa Mwaka (Person of the Year, 2014)  kutoka­na na mpango yake ya Dola za Kimarekani Bilioni Sita zitakazowezesha TANESCO kuongeza uzalishaji umeme mara tatu zaidi ya sasa  kutokana na vyanzo mbalimbali kama makaa ya mawe, gesi asilia na maji hivyo kuondokana na utegemezi wa uzalishaji umeme kwa ku­tumia mafuta.

Aidha Shirika la Maende­leo ya Petroli nchini (TPDC) limeshinda Tuzo ya transition of the year (2014) kutokana na kupiga hatua katika shughuli zake ambapo mbali ya kuwa  kuwa mdhibiti wa sekta ndo­go ya mafuta na gesi bali pia limekuwa mwekezaji baada ya kushinda tenda na kupata vitalu viwili kwa ajili ya utafiti wa mafuta na gesi nchini.

Usambazaji wa machap­isho ya TO&GY hukaguliwa na Taasisi ya Marekani ya BPA Worldwide inayokagua machapisho maalum zaidi ya 2600 katika nchi 30 Duniani yakiwemo majarida maarufu ya Toronto Star, Wall Street Journal na Gulf News.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU