JAMES MBATIA: TAMASHA LA MWAKA HUU LINA CHANGAMOTO NYINGI































LEO katika maswali matano kuelekea miaka 15 ya Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika baadaye mwaka huu hapa Tanzania,  Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi ni shabiki mkubwa wa tamasha hilo lililoasisiwa tangu mwaka 2000 ambaye anakiri aliwahi kuhudhuria baadhi ya matamasha hayo na kujionea waimbaji wa Tanzania wanavyofikisha ujumbe wa neno la Mungu kupitia uimbaji.
 
Swali: unaizungumziaje sikukuu hii kubwa kuliko zote kwa Wakristo hapa duniani, ukiwa ni muamini wa dini hiyo?
 
Jibu: Nawaomba Watanzania kujiandaa kusherehekea Sikukuu hiyo ambayo ni kubwa zaidi ya zote duniani kwani tunasherehekea kufufuka kwa Bwana Yesu Kristo aliyefufuka kwa ajili ya kuwakomboa waumini mbalimbali ulimwenguni.
 
 Swali: Nini wito wako kwa waumini katika sikukuu hiyo muhimu zaidi?
 
Jibu: Wito wangu kwa waumini kwanza ni kutambua maana ya Pasaka na kwanini tunasherehekea sikukuu hiyo adhimu hapa duniani.
 
Pili nawaomba Watanzania wenzangu kujua maana ya Pasaka kwani hata Wakristo baadhi hawatambui maana ya Pasaka na kwanini tunasherehekea sikukuu hii muhimu ya kukumbuka ufufuko wa kipenzi chetu.
 
Swali:Nini wito wako kwa Tamasha la Pasaka ambalo linatimiza miaka 15 tangu kuasisiwa kwake na Kampuni ya Msama Promotions?
 
Jibu: wito wangu kupitia Tamasha la Pasaka ambalo ni ufufuko wa  Bwana Yesu Kristo, Watanzania tulitumie kutenda mema yanayomfurahisha na kumpendeza Mungu, kwani sasa hivi kuna matukio mengi machafu yanayomuudhi na kumchukiza Mungu, hivyo ni nafasi yetu kumpigia magoti na kumuomba.
 
Kwani tamasha hilo la muziki wa Injili si la Wakristo pekee, linashirikisha mashabiki mbalimbali wa muziki huo wenye mwelekeo wa kuzungumza na Mungu kupitia Waimbaji wanaopanda jukwaani ambao wanapaza sauti zao zinazokwenda mbali zaidi kwa lengo la kumpigia magoti na kumuomba Mungu.
 
Swali: Unawaasa nini Watanzania kupitia tamasha hilo ambalo lina mlengo wa kusaidia jamii zenye uhitaji maalum kama yatima, walemavu, wajane na wenye shida zinazofanana na hizo ambazo zinahitaji msaada kutoka kwa wenye huruma kama Alex Msama?
 
Jibu: Wito wangu kwa Watanzania ni kuongeza upendo  ili kuilinda amani yetu tuliyonayo tuliyoachiwa na muasisi wa taifa hili, marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alituasa tupendane kwani hata maandiko matakatifu yanatueleza juu ya upendo baina ya wanadamu.
 
Amani na upendo linatakiwa lizingatiwe kwa sababu, tunashirikiana na nchi jirani kupitia waimbaji na hata viongozi kadhaa ambao wanashiriki kwenye tamasha hilo ambalo linakusanya nchi kadhaa za Afrika zikiwemo Afrika Kusini, Zambia, Kenya, Rwanda na moja ya bara la Ulaya ambayo ni Uingereza, jambo ambalo ni la kujivunia zaidi kwa sababu inaonesha sala zetu zinafika kwa Mungu ipasavyo kwani kadri siku zinavyozidi kwenda mbele idadi ya wageni kupitisa tamasha hilo wanazidi kuongezeka, hivyo ni nafasi yetu kuitunza na kuithamini tunu hiyo muhimu tuliyopewa na Mungu.
Kanuni ya utu, binaadamu wote ni ndugu moja, mambo ya kuuana wenyewe kwa wenyewe, uhasama, ufisadi, mauaji ya albino na machafu mengine yanayochafua taswira na uongozi wa mataifa mbalimbali hasa Tanzania iliyogubikwa na wingu hilo zito yatapungua kupitia Tamasha la Pasaka ambalo ndio nguzo kuu ya kuondoa udhaifu huo.
 
Swali: Nini changamoto iliyoko mbele hasa kwa masuala kama upitishwaji wa Katiba pendekezwa, uchaguzi Mkuu na mengineyo yanayoendelea kabla ya maendeleo hayo?
 
Jibu:Tamasha la Pasaka mwaka huu lina changamoto nyingi kwani inatakiwa tujitafakari kwa kiasi kikubwa tulipofikia na tunakokwenda kwani tunatakiwa turudi katika umoja wetu tulioachiwa na baba wa Taifa Mwalim,u Julius Kambarage Nyerere kwani Tanzania si wakabila bali ni Taifa moja, hivyo tuachane na mifumo ambayo itaondosha umoja wetu na kutugombanisha kwa kuchonganishwa na watu wachache wasioitakia mema nchi yetu.
 
Uchaguzi mkuu wa mwaka huu una changamoto nyingi sana ambazo zisisababishe tutoke kwenye mstari wa amani na upendo tulioachiwa na waasisi wetu kwa sababu ya wachache wenye uchu wa madaraka ambao watatusababishia machafuko ambayo yataigharimu nchi yetu.
 
 Wito wake kwa waimbaji wa Tanzania ni kuongeza juhudi ili kulinda na kufanikisha maendeleo ya muziki huo ambao lengo lake ni kumfikishia Mungu kilio chetu wanadam hasa kwa matukio yanayomchukiza.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.