LEO NI SIKU YA KUZALIWA YA MDAU OTHMAN MICHUZI

Napenda Kuchukua Fursa hii Kumshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma na Mwenye Kurehemu kwa kunijaalia Uhai na afya njema hadi kufikia siku hii ya leo,ambapo ninayo furaha kubwa sana kwa kuongeza namba moja katika umri wangu,kwani bila yeye hakuna kitu chochote kinachoweza kufanyika.pia nitakuwa ni mchoyo wa Fadhila iwapo sitotoa shukrani za kipekee kwa ndugu zangu woote (wakiwemo wazazi wangu wawili,Ankal Issa Michuzi,Ahmad Michuzi,Karim Michuzi,Ramadhan Michuzi,Ismail Michuzi,Ankal Macheka,Ai Michuzi,Zahra,Tatu,Sellah,Bobby,Noreen,Adam,Saleh na wengine wengi ambao sijawataja majina yenu hapa ila moyoni ninayo,na bila kumsahau mtarajiwa wangu wa ubani bi. Farida) kwa kuwa pamoja nami katika makuzi yaliyo mema hadi leo hii kufikia hapa nilipo. Tanzania Bloggers Network (TBN) pia naomba mpokee shukrani zangu za dhati kwa kuwa pamoja nami kama mwanachama hai siku zote na bila kunitupa,pia nichukue fursa hii kutoa pongezi kwa uongozi wa TBN na wanachama wenzangu kwa kuungana pamoja katika tafrija ya kihistoria  iliyotukutanisha pamoja,kiukweli ile ilikuwa ni siku muhimu sana kwetu kwa kutukutanisha pamoja na kufahamiana zaidi,ile ilikuwa ni bonge la heko kwani kuna wengine walitamani kuwa na umoja kama wetu lakini hawafanikiwi.

pia nawashukuru marafiki,jamaa zangu pamoja na Wadau woote popote pale mlipo ambao kwa namna moja ama nyingine mmekuwa ni mchango mkubwa katika maisha yangu na kunifanya kila siku niwe bize kuhakikisha libeneke halilali mpaka kieleweke.Nawashukuruni sana tena sana na Mungu awabariki nyoote. Nawapenda sana wote na tuko pamoja sana.
TEMBELEA BLOG YA MTAA KWA MTAA Inayomilikiwa na Besdei boy Othman Michuzi kwa kufuata link hii. http://othmanmichuzi.blogspot.com

Hapa ni dole tupi,nikiwa na wadau wangu Anganile na Hellen Kiwia.

WAZIRI mKUU aendelea na ZIARA MBOZI mkoa wa mbeaya

1Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na wauguzi na madaktari ya hospitali ya mkoa wa Mbeya wakati alipofika hospitalini hapo kuwaona majeruhi wa ajali ya askari wa kutuliza ghasia iliyotokea  Februari 28, 2015 kati ya Mbeyana Chuna.
(Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)
2Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimfariji WP Cecilia  Mussa mmoja wa askari waliojeruhiwa akatika ajali ya gari iliyotokea katika  kijiji cha Chang’ombe  katika barabara ya barabara ya Mbeya Chunya Machi 1, 2015. Majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Mbeya na hali zao ni nzuri.
4Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu  Pinda akimfariji WP Mwazanije Hassan  mmoja wa askari waliojeruhiwa akatika ajali ya gari iliyotokeakwenye kijiji cha Chang’ombe  katika barabara ya Mbeya Chunya Machi 1, 2015. Majeruhi hao wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Mbeya na hali zao ni nzuri.
6Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wananchi wa Vwawa , Mbozi akiwa katika ziara ya mkoa wa mbeaya Machi 1, 2015
7 8 9Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakitazama ngoma ya kabila la Wanyiha  wakati walipotembelea kiwanda cha kusindika kahawa cha CMS kilichopo Mbozi wakiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Machi 1, 2015
10Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisikiliza maelezo kuhusu utafiti wa zao la kahawa kutoka kwa  Mtafiti Charles Mwingira wakati alipotembelea kituo cha utafiti wa kahawa cha Mbimba , Mbozi machi 1, 2015.
11Waziri Mkuu, Mizengo  Pinda akikagua shamba la mfano la kahawa fupi wakati alipotembelea kituo cha utafiti wa zao la kahawa akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Machi 1, 2015
13

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua maabara ya Shule ya Sekondari ya Vwawa akiwa kayioka ziara ya mkoa wa Mbeya Machi 1, 2015. Kushoto ni Mkuu  wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro.
15Waziri Mkuu, Mizengo Pindaq akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Vwawa  baada ya kufungua  maabara zao akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya Machi 1, 2015
17Waziri Mkuu, Mizengo Pinda namkewe Tunu wakikagua sehemu ya shehena ya mahindi iliyohifadhiwa nje ya maghala ya NFRA, Vwawa, Mbozi Machi 1, 2015

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*