Mama wa Katibu wa Mbunge afariki Dunia, wilayani Kibaha mkoani pwani


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
…………………………………………………….
MAMA wa Katibu wa Mbunge wa Viti Maalum Al Shaimar Kweigyir
Semeni Kingaru, anayeitwa Kibibi Haji Pembe, amefariki Dunia leo saa tano
asubuhi akiwa na umri wa miaka 80.
Semeni Kingaru kulia ambaye ni Katibu wa Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaimar Kweigyir, akiwa na mama yake mzazi Bi Kibibi Haji, ambaye amefariki Dunia leo asubuhi, wilayani Kibaha, mkoani Pwani.
 
Mama huyo amefariki nyumbani kwake kijiji cha
Misugusugu,wilayani Kibaha, mkoani Pwani, baada ya kuugua kwa muda mrefu.
 
Mtoto wa marehemu huyo Kingaru ambaye ni Katibu wa mbunge Al
Shaimar aliuambia mtandao huu kuwa mama yake atazikwa kesho saa 10 jioni kijijini
hapo kwa ajili ya kumsitiri.
 
Alisema kuwa kwa wanaopenda kushiriki kwenye msiba huo
watalazimika kushuka katika kituo cha kijiji cha Misugusugu ambapo ndipo sehemu
atakapozikwa marehemu mama yake.
 
Msiba huo wakati unatokea, Kingaru alikuwa nchini Uganda
katika majukumu yake na kulazimika kusitisha shughuli hizo kwa ajili ya kuwahi
msiba wa mama yake.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.