MBUNGE FILIKUNJOME ATIMIZA PIA AHADI YA UJENZI WA DARAJA MTO KITEWAKA KWA TSH MILIONI 248, ASAIDIA VIFAA VYA UJENZI KWA TSH MILIONI 2480


 Mbunge  wa  jimbo la  Ludewa  Deo Filikunjombe wa pili   kushoto na viongozi wa Halmashauri  wakikabidhiana daraja la mto Kitewaka kwa  ajili ya  kujengwa kisasa baada ya  serikali  kukabidhi fedha za ujenzi huo Tsh miloni 240
 Mbunge  Filikunjombe akilitazama daraja la mbao la mto Kitewaka ambalo litajengwa  kisasa 


 Wannchi  wa  kijiji  cha Maholong'wa  wakimpongeza  mbunge  Filikunjombe kwa kutimiza ahadi yake
 Waumini  wa  kanisa la Anglikana Maholong'wa Ludewa  wakimkabidhi zawadi mbali mbali mbunge Filikunjombe baada ya  kuwasaidia bati na  saruji  ya kutosha  kujenga kanisa  jipya
 Viongozi wa kanisa la Anglikana na wa CCM Ludewa  wakiongozana na mbunge Filikunjombe  mwenye kofia
 Mbunge  Filikunjombe akisaidi kupalilia mahindi katika shamba la mchungaji wa kanisa la Anglicana Maholong'wa baada ya  kufika  kusaidia ujenzi  wa kanisa  hilo
 Mkutano wa mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe na  wanakijiji  wa Maholong;wa
 Mzee  wa  kanisa la E.A.G.T Maboga  Ezekia Mhagama  (kulia)akimwombea  dua  mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe baada ya  kutoa misaada  mbali mbali ya ujenzi na  kujitolea kinanda  kwa  kanisa  hilo vyote  vikiwa na thamani ya zaidi ya Tsh milioni 11  wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Maholong'wa
Mkurugenzi  Ludewa Bw Waziri akizungumza katika mkutano  wa mbunge Filikunjombe
 Wananchi  wa Maholong'wa wakimpokea mbunge  wao
 Katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Njombe Bw Honoratus Mgaya  akiwahutubia  wananchi wa Maholong'wa

Na matukiodaimaBlog.
MBUNGE wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe ametimiza ahadi yake ya ujenzi wa daraja la mto  Kitewaka katika kijiji cha Maholong'wa kata hiyo ya Ludende baada  ya serikali kumpatia  kiasi cha Tsh milioni 2480 zilizokuwa zikihitajika kwa ajili ya ujezi wa daraja hilo .

Mbali ya  kutimiza ahadi hiyo ya  daraja  pia amechangia vifaa vya ujenzi vyeye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 11 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika shule ya Msingi Maholong'wa na ujenzi wa kanisa la Anglikana kijiji cha Maholong'wa kata ya Ludende wilayani Ludewa mkoani Njombe .

Akizungumza na wananchi hao leo mbunge Filikunjombe alisema kuwa kuwepo bungeni ni heshima ya wana Ludewa na kuwa hata vurugu kubwa ambazo amekuwa akizifanya bungeni si kwa maana nyingine zaidi ya kupigania maendeleo ya wananchi wake.

Hata   hivyo  aliipongeza  serikali  kuwa  kusaidia  kutoa  fedha   hizo  kwa  wakati kwa ajili ya  kuanza ujenzi hao na  kuwa  iwapo  asingefuatilia kwa karibu   serikalini ama angekuwa wa kulala bungeni yawezekana  fedha kwa  ajili ya ujenzi wa daraja   hilo zisingetolewa sasa.

 “wapo wabunge wengine ambao kazi yao ni kusinzia tu na wala haulizi swali …..ila huo pia ndio uwakilishi wake ulipoishia …..mimi silali kule bungeni mimi ninawatetea na kuwapiganieni kwa kulia nalia na kwenye kugombana nagombana pia pale kwenye kunyenyekea nanyenyekea….. napenda kuwaelezeni kuwa kazi ambayo mlinipa kuwawakilisha bungeni naitumia vema hadi sasa sijakwama kuwatumikia ….nilisema mwanzoni mimi navurugu bungeni ila ni vurugu za kimaendeleo”

Filikunjombe alisema kuwa waakati akiomba kuwa mbunge wa Ludewa alitaka kuwawakilisha bungeni na kushirikiana nao katika shughuli za kimaendeleo hivyo angekuwa mbunge wa ajabu kama angekuwa mbali na shughuli za kimaendeleo katika jimbo lake .

 Alisema wakati akigombea ubunge mwaka 2010 aliwaahidi wananchi wa kata la Ludende kuwajengea daraja la kisasa zaidi katika kijiji cha Maholong'wa ili kuchochea kasi ya maendeleo katika kata ya Ludende na kata za jirani ,ahadi ambayo sasa anaitimiza kwa kumpata mkandarasi atakayejenga daraja hilo kwa Tsh milioni 248 na ujenzi wake utaanza mara moja baada ya mvua kutulia . “

"Mimi nataka ujenzi huu uanze mara moja kwani kama shida wananchi wangu mmetesema sana hivyo sasa nataka iwe basi matesa na sitapenda kuona Halmashauri inaziweka pesa hizo pasipo kutumika kwa kazi iliyokusudiwa fedha  za ujenzi huu zimetoka serikalini baada ya kuwabana zaidi"

Alivitja vifaa hivyo kuwa ni bati 200 na saruji 200 pia kinanda kwa kanisa la E.A.G.T na vifaa mbali mbali vya michezo pamoja na kuwakodia usafiri kutoka Dar es Salaam hadi kijijini hapo kwa ajili ya kusafirisha vifaa hivyo.

 Awali viongozi wa madhehebu ya dini na vyama vya siasa katika kata ya Ludende wilaya ya Ludewa wamepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe na kuwa hawahitaji kubadili tena wabunge kama nguo .

 Huku mwenyewe akidai kuwa yeye si mbunge wa kusinzia bungeni ni makini katika kuwawakilishi wananchi wake na kuwa ana vurugu sana bungeni ila vurugu zake ni za kimaendeleo si vinginevyo.

Wakishukuru mara baada ya kuwakabidhi mkandarasi wa kuanza ujenzi wa daraja , pamoja na saruji na bati kwa ajili ya kuchangia miradi mbali mbali ya kimaendeleo katika kata hiyo na ujenzi wa kanisa jipya ya Anglicana kijiji cha Maholong’wa.

 Viongozi hao akiwemo mzee wa kanisa la E.A.G.T Mboga Bw Ezekia Mhagama na mkuu wa shule ya msingi Maholong’wa Bw Damas Malihayi walisema kuwa maendeleo makubwa yanayoendelea kuonekana katika wilaya ya Ludewa ni jitihada kubwa ambazo zinafanywa na mbunge huyo na hivyo wao kama viongozi wa dini kazi kubwa ni kuzidi kumwombea afya njema ili aendelee kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa vipindi vingine zaidi.

 Alisema mzee huyo wa kanisa la E.A.G.T kuwa matumaini ya wananchi wa Ludewa yamekuwa makubwa zaidi dhidi ya mbunge wao kutokana na sura ya Ludewa kwa sasa baada ya mateso ya miaka zaidi ya 50 ya Uhuru bila kuwepo kwa maendeleo yanayoonekana ila toka alipoingia mbunge Filikunjombe mwaka 2010 wananchi wa Ludewa ndipo walipata uhuru wao na kuwa wao wanajiona kama miaka hii mitano toka walipomchagua mbunge huyo kuwa mbunge wao ndipo wao walipopata uhuru wao.

“Tunatambua nchi yetu ilipata uhuru mwaka 1961 kwa maeneo mbali mbali ya nchi wananchi wake kusogezewa huduma mbali mbali zikiwemo barabara za lami ila sisi Ludewa lami tumeanza kuiona mwaka jana na kama huku Maholong’wa daraja ambalo ni tegemeo kubwa kwetu lilikuwa la mbao hadi sasa ambapo mbunge wetu ametusaidia kutafuta pesa ya kujenga daraja la kisasa na huu ndio uhuru wetu “

Mhagama alipongeza pia kwa msaada wa saruji na bati za kutosha kukamilkisha ujenzi wa kanisa la Anglicana na msaada wa kinanda kwa kanisa lake la E.A.G.T kuwa ni mbunge pekee kusaidia jamii nzima ya Ludewa pasipo kutazama masuala ya itikadi zao .

 Hivyo allisema kwa wananchi wa Ludewa hawana sababu ya kuendelea kubadili badili wabunge kwa sasa kwani utendaji kazi wa mbunge Filikunjombe umewakuna wengi na hivyo kazi kubwa kwao ni kuendelea kumuunga mkono kwa kumpitisha tena na tena kuwa mbunge wao .

 Mkuu wa shule ya Msingi Maholong’wa Bw Malihayi alisema kuwa kuna haja ya wana Ludewa kushikamana na kuona hawampotezi mbunge huyo na badala yake kuzidi kumpa ushirikiano zaidi.

Kwa upande wake Paschal Kayombo akizungumza kwa niaba ya vijana wa kata hiyo alisema kuwa kero kubwa ya vijana ilikuwa ni daraja hilo la mto Maholong’wa ambalo kwa sasa limekwisha patiwa ufumbuzi na kuwa vijana kwa sasa wanaimani kubwa na utendaji kazi wa mbunge huyo.

Katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya akiwahutubia wananchi hao alisema kuwa CCM ni chama kizuri sana ila wanaofanya wananchi kukichukia chama ni baadhi ya viongozi wakiwemo wabunge ambao wameshindwa kuwatumikia vema wananchi wao.

Kwani alisema iwapo kila mbunge atafanya kazi kwa kujituma kama ilivyo kwa mbunge Filikunjombe uwezekano wa kata ama majimbo kuchukuliwa na vyama vya upinzani usingekuwepo ila wanaopigia kura wapinzani ni wana CCM ambao wamechoshwa na uwajibikaji mbovu wa wale waliowachagua.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI