SHULE YA IDODI YA IRINGA YATEKETEA TENA

 Bweni  la  wasichana katika  shule ya  sekondari Idodi  wilaya ya  Iringa  likiwa  limeteketea kwa  moto jana ,picha  nyingine wazazi na  wanafunzi  wakiwa nje ya Bweni   hilo ,na  picha  nyingine na  mmoja kati ya majeruhi  katika  tukio hilo la Moto  akiwa  katika  kituo cha afya  Idodi (picha na  Francis Godwin Blog)
Mmoja wa wanafunzi akiokolewa

Na Francis  Godwin,Iringa

UKIWA  umepita  mwezi  mmoja   toka  sehemu ya bweni  la  wasichana  katika  shule ya  sekondari Idodi  wilaya ya  Iringa mkoani  Iringa  kuteketea kwa  moto ambao  chanzo  chake  kilitajwa  kuwa ni  hitirafu ya  umeme , moto mwingine  tena  umeibuka na  kuteketeza  sehemu ya bweni   hilo iliyobaki  huku  wanafunzi  zaidi ya 14  wakijeruhiwa .

Wakielezea  juu ya  tukio hilo  wanafunzi  wa  shule   hiyo  walisema  kuwa  moto  huo ulianza  kuteketeza bweni hilo  juzi (jumapili) majira ya saa 9 Alhasiri  wakati  wanafunzi  wote  wakiwa  madarasani  wakiendelea  kujisomea.

Alisema  mmoja  kati ya  wanafunzi  kuwa  wakiwa katika mdahalo  wa  wanafunzi  shuleni  hao  walisikia  kelele  kutoka  nje ya darasa   juu ya  kuwaka  kwa  bweni  hilo ila hawakuweza  kutilia manani sana  wakijua ni utani  ila kulingana na  kelele  zilivyozidi ndipo   walilazimika  kutoka kwenda eneo la  bweni hilo la Benjamini Mkapa  ambalo  hutumiwa na  wasichana na  kukuta  moto  ukiwa  umeshika kasi  zaidi na hivyo  kuanza  kuuzima  moto   huo kwa  kushirikiana na  walimu na baadhi ya  wananchi  waliofika kwa  wakati  eneo hilo.

Hata  hivyo   wanafunzi hao  ambao  hawakutaja  kutajwa majina  yao   kiusalama  walisema  kuwa  chanazo  cha  moto  huo inaonyesha  ni hitrafu ya  umeme inayosababishwa na baadhi ya  wanafunzi  wenzao ambao  si  waaminifu  wenye tabia ya  kuchaji  simu  zao bwenini kwa  kuchubua  nyaya za  umeme .

Kwani  walisema  kuwa  mabweni hayo hayana  sehemu maalum  za  kuchajia  simu  huku  asilimia  kubwa ya  wanafunzi wanatumia  simu  hivyo  kutokana na kuhofia  kukamatwa na  simu  wamekuwa wakitumia  muda  wa kwenda madarasani kwa  ajili ya  kuchaji  simu  zao kwa  siri kubwa .


MKuu  wa   shule   hiyo Bw  Christopher Mwasomola  alisema  kuwa  kwa  kawaida  wanafunzi  wa  shule   hiyo hawaruhusiwi  kuwa na  simu  japo siku  za  jumamosi na  jumapili  uongozi  wa  shule   hiyo  huwa  unawapa   simu  wanafunzi  kwa  ajili ya  kuwasiliana na jamaa  zao.

"Kusema  chanzo  cha  moto  huu ni  simu bado  siungi  mkono kwani  hakuna   sehemu ya  kuchajia  simu katika mabweni ya  wanafunzi hivyo  bado  tunaendelea na uchunguzi  zaidi  ili  kujua  chanzo hasa cha  moto  huu  "

Alisema   kuwa katika  tukio  la moto  lililotokea  mwezi  uliopita  jumla ya  madogoro 190  yaliteketea  kwa  moto na   katika  tukio  hilo la  pili  jumla ya madogoro 48 ambayo ni mali ya  wanafunzi pamoja na mashuka yameteketea kwa  moto na  vitu  mbali mbali  vya  wanafunzi hao   huku hasara  nyingine iliyojitokeza  ikiwemo  ya jengo   hilo .

Kwa  upande  wake  mkuu  wa wilaya ya  Iringa Bi  Angelina Mabula  akizungumza na  wananchi  wa  Idodi  na  walimu  wa shule   hiyo  alitaka  kufanyike kwa uchunguzi  wa  kina ila  kuweza  kujua  chanzo  cha matukio  hayo  mfululizo katika shule  hiyo  ikiwa ni pamoja na  kuchunguza umiliki wa ardhi  hiyo  ambayo shule   hiyo  imejengwa kama  wapo  wenye dukuduku basi  kukaa nao  ili  kuondoa  tofauti  zilizopo.

Wakati  huo  huo  mkuu  huyo  wa  wilaya  ameagiza  shule  hiyo  kufungwa kwa  muda  wa wiki  mbili  ili  kufanya uboreshaji  wa bweni  hilo ambalo  limeteketea  lote kwa  moto na kuwaomba  wananchi  kujitolea  nguvu  zao  ili  kuharakisha ukarabati  wa  jengo  hilo.

Mbunge  wa  jimbo la Isimani Wiliam  Lukuvi mbali ya  kuwapa  pore  walimu na  wanafunzi  wa shule   hiyo kwa  tukio   hilo bado alisema  kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa  tukio  hilo na kwa  sasa ataungana na  wananchi  wa  Idodi  katika uboreshaji wa  jengo  hilo  ili  wanafunzi waweze kurejea kwa  wakati .

Akizungumza na  mwandishi  wa habari hizi kwa  njia ya  simu Bw  Lukuvi  alisema anachokifanya kwa  sasa ni kutafuta  wahisani  mbali mbali  ili  kufanikisha  ukarabati  wa  jengo   hilo kwa  kushirikiana na  wananchi  wake .
MWISHO

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.