TBL YATOA MSAADA WA SH. MIL. 56 ZA KISIMA CHA MAJI MKURANGA


 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, Luteni Mstaafu Abdallah Kihato (wa pili kulia), akipokea Hundi ya Sh. Milioni 56 kutoka kwa Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya Kusini, Bw. Victor Kavishe (wa pili kushoto) kwa ajili ya kusaidia mradi wa maji katika Kijiji cha Magoza, kilichoko Kata ya Kiparang'anda. Kushoto ni Meneja Mahusiano wa TBL, Bi. Emma Urio na Diwani wa Kata hiyo, Bi. KAru Karapina. (Na Mpigapicha Wetu)
  Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kanda ya Kusini, Bw. Victor Kavishe (wa pili kushoto, akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, Luteni Mstaafu Abdallah Kihato, Hundi ya Sh. Milioni 56 zilizotolewa na Kampuni hiyo kwa ajili ya kusaidia mradi wa Maji katika Kijiji cha Magoza, kilichoko Kata ya Kiparang'anda. Kushoto ni Mkuu wa Mahusiano TBL,
Bi. Emma Urio na Diwani wa Kata hiyo, Bi. Karu Karavina. (Na Mpigapicha Wetu)
 Akionesha Hundi aliyopewa na TBL

 Diwani wa Kata ya Kiparang'anda, iliyoko Mkuranga, mkoani Pwani, Bi. Karu Karavina akiishuikuru Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), baada kampuni hiyo kutoa Hundi ya Sh. Milioni 56 za mradi wa maji katika kijiji cha Magoza.. Walioketi kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Luteni Mstaafu Abdallah Kihato na Meneja Uhusiano TBL, Emma Urio.
 Afisa Uhusiano wa TBL. Bi. Doris Malulu akiungana na kinamama wa Kijiji cha Magoza kuomba dua ili maji yapatikane katika kijiji hicho.
 Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bi. Emma Urio akizungumza na wananchi wa Magoza, kabla ya kampuni hiyo kukabidhi sh. milioni 56 za mradi wa maji.

 Mkurugenzi wa Kampuni ya GCL, Bw. Gerald Mosha (kushoto) akiomba dua pamoja na wananchi wa Kijiji cha Magoza kwa ajili ya kufanikisha mradi wa maji.
Diwani wa Kata ya Kiparang'anda Bi. Karu Karapina akikabidhi zawadi mbalimbali zilizotolewa na wananchi wa Magoza kwa ajili ya TBL.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA