WATU SABA WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA KUHUSIKA KUTEKA NA KUKATA KIGANJA CHA MTOTO ALBINO SUMBAWANGA
Jeshi la polisi mkoani rukwa linawashikilia watu saba hadi sasa, kwa
tuhuma za kuhusika na kitendo cha kikatili cha kukata kiganja cha mkono
wa kulia, cha mtoto mwenye ulemavu wa ngozi Baraka Cosmas Lusambo mwenye
umri wa miaka sita, katika kitongoji cha kikonde kata ya kipeta wilaya
ya sumbawanga vijijini, ambapo pia katika tukio hilo wamemjeruhi mtoto
huyo mkono wa kushoto.
Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa rukwa kamishna msaidizi wa polisi Leons Rwegasira, amesema
wamefanikiwa kuwakamata watu hao kufuatia msako mkali, mara tu baada ya
kutokea tukio hilo kwenye kitongoji hicho cha kikonde, ambacho kinakuwa
na wakazi wakati wa msimu wa kilimo na kiangazi watu wanahama tena,
katika familia yenye watoto wengine watatu wenye ulemavu wa ngozi.
ACP.Rwegasira
pia amesema kwenye msako huo mkali, wamefanikiwa kuwakamata watu wanane
wanaojihusisha na uganga wa jadi na upigaji wa ramli chonganishi,
ambacho ni chanzo kikubwa cha kusababisha vifo na kujeruhiwa watu wenye
ulemavu wa ngozi kwa imani za kishirikina.
Mtoto
baraka na mama yake mzazi wamelazwa kwene hospitali ya rufaa ya jijini
mbeya, wakitibiwa majeraha waliyoyapata wakati wa purukushani za
kumshambuliwa mtoto huyo.
No comments:
Links to this post