Alshabaab washukiwa kumteka nyara Chifu


Alshabaab wadaiwa kumtekanyara Chifu wa kaunti ya Mandera
Wanamgambo wanaoaminika kuwa Al Shabaab wamemteka nyara chifu na gari la miraa katika eneo la Arabia, kaunti ya Mandera.
Shambulizi hilo limetokea mapema siku ya Alhamisi , na maafisa wa usalama wako katika harakati ya kuwaokoa manusura waliotekwa nyara.
Viongozi wamesema washambuliaji walionekana kufahamu eneo hilo na pia Chifu waliyemteka nyara. Inasemekana kuwa Chifu huyo alikuwa akielekea Mandera wakati wa shambulizi hilo.
Awali katika idhaa yaa BBC Somali tuliweza kuzungumuza na mwakilishi wa kaunti katika wadi ya Arabia na kaweza kutuhakikishisa shambulizi hilo na vile vile alisema kuwa wanashuku wanamgambo wa Alshabab ndio waliofanya kitendo hicho.
Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kutoka serikali kuhusiana na utekaji nyara na muda mfupi uliopita kulikuwa na taarifa isiyo thibitishwa kuwa chifu huyo ameuwawa na Alshabaab.
Kutokana na swala hili la Usalama wanasiasa jimbo la Mandera waliweza kuongea na wanahabari huku wakilaani kitendo hicho huku wakihimiza serikali kuimarisha usalama katika mkoa wa kaskazini mashariki mwa Kenya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU