CAF yataja wapinzani wa Twiga - Afrika


Twiga stars viwanjani na shepolopolo ya Zambia
Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limetaja timu zitakazokwaana na timu ya Twiga Stars ya Tanzania katika fainali za soka za wanawake za Michezo ya Afrika itakayofanyika mwezi Septemba nchini Congo Brazzaville.
Twiga Stars imefanikiwa kucheza fainali hizo baada ya kuitoa timu ya Zambia (Shepolopolo).
Kwa mujibu wa CAF, timu zitakazochuana katika michezo hiyo baada ya kufuzu ni wenyeji Congo (Hosts), Cameroon, Ivory Coast (ambayo imefuzu baada ya Guinea Bissau kujitoa), Ghana, Misri, Nigeria, Afrika ya Kusini na Tanzania
Timu hizo zimefuzu baada ya kupata matokeo yafuatayo:
Nigeria 8-0 Mali (1-1- matokeo ya mechi ya kwanza)
Tanzania 2-3 Zambia (4-2)
Senegal 1-2 Egypt (0-0)
Afrika ya Kusini 5-0 Botswana (0-1)
Cameroon 2-1 Ethiopia (2-1)
Zimbabwe 2-2 Ghana (1-2)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI