LIGI KUU YA VODACOM KUENDELEA WIKIENDI HII


Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania inatarajiwa kuendelea wikiendi hii katika viwanja sita tofauti nchini, viwanja vinne vikitimua vumbi kesho jumamosi, na michezo miwili kuchezwa siku ya jumapili.

Jumamosi JKT Ruvu watakua wenyeji wa Coastal Union katika Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es salaam, huku wakata miwa wa Kagera Sugar wakiwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Timu ya Mtibwa Sugar watawakaribisha Azam FC kwenye uwanja wa Manungu-Turiani mjini Morogoro,nayo  Ndanda FC watakua wenyeji wa timu ya Tanzania Prisons mjini Mtwara katika uwanja wa Nangwanda Sijaona.

Ligi hiyo itaendelea siku ya jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Young Africans watawakaribisha timu ya Mbeya City kutoka mkoani Mbeya, huku mjini Shinyanga katika uwanja wa Kambarage wenyeji timu ya Stand United wakiwakaribisha maafande wa  timu ya Polisi Morogoro.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


-- 
Best Regards,
 
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER
T: +255 22-2861815  I F: +255 22-2861815  I C: +255 713 455970 
A:I P.O.BOX 1574 Karume Memorial Stadium /Shaurimoyo/Uhuru Street I Dar es salaam I Tanzania  
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.