UTENDAJI KAZI WA FILIKUNJOMBE WAWAVUTIA WANANCHI WAKE WASEMA HAWAHITAJI MBUNGE ZAIDI

      

 
Mbunge  wa Ludewa Deo Filikunjombe akishirikiana,viongozi wa CCM , wananchi na mafundi  wa mradi wa umeme kubeba nguzo za  umeme katika  kitongoji cha Ngalawale Ludewa kijijini kama  sehemu ya kuhamasisha wananchi kushiriki maendeleo
 
Mbunge Filikunjombe wa kwanza  kulia na katibu mwenezi wa CCM mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya wa  kwanza  kulia wakishirikiana na mafundi wa maradi wa  umeme vijiji kuvuta kama kwa ajili ya kusimamisha nguzo ya  umeme
 
 mbunge Filikunjombe kulia  na diwani wa kata ya Ludewa Monica Mchilo wakifukia  nguzo ya  umeme
Wananchi na  mbunge  wakisaidiana kufukia nguzo ya  umeme
 
wananchi na mafundi wa  umeme  wakijiandaa kubeba  nguzo

mbunge Filikunjombe  akishiriki  kubeba  nguzo ya  umeme

wananchi na  mbunge Filikunjombe wakiwa  wamebeba nguzo ya  umeme
 
 
katibu  mwenezi wa CCM mkoa wa NJOMBE Honoratus Mgaya akichimba shimo la nguzo ya umeme
 
mbunge Filikunjombe akiwa  chini ya shimo akishiriki  kuchimba shimo la nguzo ya  umeme  kitongoji cha ngalawale  kijiji  cha ludewa wengine ni diwani wa kata ya  Ludewa MONICA MCHILO ,katibu mwenezi wa ccm mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya na katibu mwenezi  wa CCM ludewa FELIX Haule  wakishirikiana na mbunge  wao
 
 mbunge Filikunjombe akitoka  katika  shimo baada ya  kumaliza  kuchimba  shimo  moja la mfano kama kuhamasisha wananchi kushiriki katika maendeleo 
……………………………………………………………………………………………………………………….
 
Na MatukioDaima BLOG Ludewa
WANANCHI
wa  Ngalawale kata ya Ludewa  wilaya  ya Ludewa  mkoani Njombe
wameelezwa kufurahishwa na jitihada  za  kimaendeleo  zinazofanywa na
mbunge  wao Deo Filikunjombe na kukionya chama   cha  mapinduzi (CCM)
katika wilaya   hiyo kutowaletea mgombea mwingine  wa ubunge  zaidi ya
Filikunjombe.
 
Akizungumza
kwa  niaba ya  wananchi wa  kata  hiyo ya Ludewa  diwani wa kata  hiyo
Monica  Mchilo alisema   kuwa toka  jimbo  hilo la Ludewa kuanza kuwa na
wabunge pamoja na  kuwa  kila mmoja ana jambo la  kukumbukwa ambalo
amepata  kulifanya katika   jimbo hilo ila hakuna hata  mbunge  mmoja
kati ya wabunge  zaidi ya  watano waliopata  kuongoza  Ludewa  ambae
amepata kutekeleza ahadi zake hata robo ya ahadi  alizopata   kutoa.
 
Diwani
Mchilo alitoa kauli   hiyo leo  wakati wa mkutano wa hadhara  wa
mbunge Filikunjombe  kuwapongeza  wananchi  hao kwa kukamilisha
uchimbaji  wa mashimo ya nguzo  za  umeme katika  kijiji  chao .
 
Alisema
kuwa wakati mbunge huyo  akiingia madarakani  mwaka 2010 moja kati ya
ahadi yake ni kuhakikisha wananchi  wa  vijijini ambao  wapo pembezoni
na mji  wa Ludewa  wanapatiwa  umeme na  kuwa kabla ya kumaliza  muda
wake wa ubunge tayari ahadi  hiyo  imetekelezeka na ahadi nyingine
nyingi alizopata  kuzitoa  kwa  wananchi  wa  jimbo   hilo.
 
Hivyo
alisema kuwa inapendeza  kuwa wana Ludewa  kuendelea kumpa muda zaidi
mbunge  Filikunjombe  ili azidi  kuleta maendeleo zaidi katika  jimbo
hilo badala ya kuendelea  kubadili   wabunge kila   wakati jambo
linalokwamisha maendeleo ya jimbo hilo na kuishia kuwapata   wabunge
wasio na mapenzi mema na maendeleo ya wananchi.
 
‘Ludewa
kwa  miaka  mingi   tumeteseka  kwa  kumkosa  mbunge  mwenye  uchungu
wa  maendeleo ya  wananchi  wa jimbo hilo ila  kwa mara  ya kwanza
Mungu  ametupatia mbunge mwenye uchungu  wa kweli na maendeleo  yetu
hivyo lazima tumkumbatie azidi  kutawala daima’
 
 
Akielezea
kuhusu  miradi mbali mbali iliyofanyika katika  kata  yake alisema
kuwa awali umeme ulikuwepo mjini Ludewa  pekee  kwa  kipindi chote
toka  nchi ipate  uhuru  wake mwaka 1961 na  kuwa umeme  huo  aliuleta
aliyekuwa  mbunge  wao stanley kolimba ambae  kwa  sasa ni mwenyekiti
wa CCM wilaya ila  kwa  kipindi cha Filikunjombe  vijiji  zaidi
vimeendelea  kupatiwa umeme na maendeleo mengine  mengi  ikiwemo
barabara ya lami Ludewa mjini.
 
Diwani
huyo aliwataka  wananchi  wa Ludewa kutoyumbishwa na wale wote wenye
uchu wa madaraka ambao wapo kwa  maslahi yao  na badala yake  kubaki
njia kuu kwa  kuendelea kuwa na mbunge  Filikunjombe kwa  kipindi
kingine  zaidi.
 
‘kwa
kuwa utaratibu wa  chama ni kutangaza uchaguzi wa  kura za maoni ila
kama ingeruhusiwa tungezuia chama kutoa fomu kwa wagombea wengine wa
ubunge ….lakini tunakuhakikishia wewe endelea kufanya maendeleo bila
hofu kwani ni mbunge wetu wa 2015-2020 na zaidi hadi mwenyewe
utakaposema basi sisi tupo na wewe’
 
Katibu
mwenezi  wa CCM mkoa  wa Njombe Honoratus Mgaya  alisema mbali ya
kubahatika   kuwa katibu mwenezi  wa mkoa  wa Iringa uliokuwa na wilaya
zaidi ya 6 na majimbo zaidi ya 10 hakupata  kuona  mbunge anayejituma
kama Filikunjombe na  kuwa mbali ya  ubunge  wake  kuwanufaisha
wananchi  wa Ludewa ila bado amefanikiwa  kuutangaza  mkoa  wa Njombe na
kuwa moja kati ya  wabunge wa mfano katika bunge.
 
Mgaya
alisema  kama wabunge wote wa CCM wangeifanya kazi  ya  kuwatumikia
wananchi kama anavyofanya mbunge  huyo  wa Ludewa uwezekano wa
wapinzani kwenda bungeni ungekuwa mdogo  zaidi  na kuwa chuki ya
wananchi dhidi ya CCM  ni  kutokana na baadhi ya wabunge ,madiwani na
viongozi wengine wa umma kushindwa kuwajibika katika kuwatumikia
wananchi .
 
Nae
mbunge Filikunjombe akiwashukuru wananchi hao  alisema  kuwa moja kati
ya ndoto  yake ni kuona wananchi  wa Ludewa wanaungana na watanzania
wengine  katika kunufaika na uhuru wao kwa  kupatiwa umeme na huduma
nyingine za kijamii.
 
Kwani
alisema amepata  kupigania  kuona wananchi  wa vijiji 14 vya jimbo la
Ludewa ambao walikuwa  gizani kwa muda  wote wa nchi ilipopata uhuru
wanapatiwa umeme kabla ya kumaliza kipindi chake  cha kwanza na ubunge
na kuwa kamwe hatakubali  kuona mtu yeyote anashiriki kukwamisha ndoto
yake  hiyo ya  kuwaletea maendeleo wananchi .
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA