FIGO AJITOA KINYANG'ANYIRO CHA URAIS FIFA

MWANASOKA wa zamani wa kimataifa wa Ureno, Luis Figo ametangaza kujitoa kwenye mbio za Urais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu. 

Rais wa Chama cha Soka Uholanzi, Van Praag naye mapema alijitoa na kutangaza kumuunga mkono Prince Ali bin Al Hussein, ambaye atapambana na Rais wa sasa, Sepp Blatter.
Mwanasoka huyo wa zamani wa kimataifa wa Ureno amesema katika taarifa aliyotoa kwenye ukurasa wake Facebook kwamba; "Nimefanya uamuzi wangu, sitasimama katika huo unaoitwa uchaguzi huo wa FIFA. 
Figo amesema kwamba alikubali kugombea Urais kwa FIFA inahitaji mabadiliko hayo haraka, lakini ameshuhudia mambo ambayo yanaweza kumtia aibu yeyote mmoja anataka anataka kuikomboa soka.
Luis Figo announced his intention to stand for the FIFA presidency on Wednesday
Luis Figo ametangaza kujitoa kuwania Urais wa FIFA 
Figo won 127 international caps for his native Portugal and scored 32 goals
Figo aliichezea timu yake ya taifa Ureno mechi 127 na kuifungia mabao 32 

WASIFU WA LUIS FIGO

Umri: Miaka 42 
Klabu alizochezea:
Sporting (1989–1995) - mechi 137, mabao 16
Barcelona (1995–2000) - mechi 172, mabao 30
Real Madrid (2000–2005) - mechi 164, mabao 38
Inter (2005–2009)- mechi 105, mabao 9
Mechi za kimataifa: 
Mechi 127 Ureno, mabao 32
Mataji na tuzo: 
Barcelona - La Liga mawili, Copa del Reys mbili, Kombe la Washindi la UEFA moja, UEFA Super Cup moja,
Real Madrid - La Liga mawili, Ligi ya Mabingwa moja, UEFA Super Cup moja
Inter Milan - Serie A manne, Coppa Italia moja
Tuzo binafsi: 
Mwanasoka Bora wa Ureno kuanzia 1995 hadi 2000
Ballon d'Or mwaka 2000

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI