JK ATEUA MAKATIBU TAWALA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewateua makatibu tawala wa Mikoa ya Singida na Shinyanga kuanzia jana, Jumatatu, Mei 25, 2015.
Katika uteuzi huo, Rais Kikwete amemteua Ndugu Festo Luganda Kang’ombe  kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida na Ndugu Abdul Rashid Dachi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga.
Kabla ya uteuzi wake, Ndugu Kang’ombe alikuwa Mkurugenzi wa Halmashuri ya Kibaha, Mkoa wa Pwani wakati Ndugu Dachi alikuwa Katibu Tawala Msaidizi, Sekretarieti ya Mkoa wa Lindi.
Ndugu Kang’ombe anachukua nafasi ya Ndugu Liana Hassan ambaye amestaafu utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria tokea Machi, mwaka huu, na Ndugu Dachi anachukua nafasi ya Ndugu Anselm Tarimo ambaye naye alistaafu utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria Januari 22, mwaka huu, 2015.
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.

26 Mei, 2015

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.