Katibu Tawala wilaya ya Masasi, Dunford Peter akimwonyesha ramani Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu ya sehemu ya mto huo, wakati waziri huyo alipotembelea mto Ruvuma katika kijiji cha Manyuli ambako alitembelea.
Diwani wa Nhavila, wilayani Masasi Meja Ramadhan Chilumba akimwongoza Waziri wa maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alipotembelea mto Ruvuma katika kijiji cha Manyuli wilayani Masasi, mpakani na Msumbiji alikokwenda kutoa kifutajasho kwa watu waliojeruhiwa na kuuawa na mamba katika mto huo.
Diwani wa Nhavila, wilayani Masasi Meja Ramadhan Chilumba akimwongoza Waziri wa maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alipotembelea mto Ruvuma katika kijiji cha Manyuli wilayani Masasi, mpakani na Msumbiji alikokwenda kutoa kifutajasho kwa watu waliojeruhiwa na kuuawa na mamba katika mto huo.
Wanakijiji wa Manyuli, wilayani Masasi wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alipozungumza nao jana, alitembelea watu waliojeruhiwa na wengine kuuawa na mamba, alipokwenda kutoa kifuta machozi kutoka wizarani kwake.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizungumza na wanakijiji wa Manyuli wilayani Masasi ambako alitembelea watu waliojeruhiwa na wengine kuuawa na mamba, alipokwenda kutoa kifuta machozi kutoka wizarani kwake.
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, amewaagiza askari na maofisa wa wanyamapori nchini kuwavuna mamba wanaoua na kujeruhi wananchi katika maeneo mbalimbali nchini.
Alitoa agizo hilo wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Manyuli wilayani Masasi mkoani Mtwara, alipokwenda kukagua madhara yatokanayo na mamba katika Mto Ruvuma.
Kauli ya Nyalandu imetokana na kilio cha Mbunge wa Masasi, Mariam Masembe na wananchi wake kuwa mamba hao mbali na kuua na kujeruhi wananchi, pia wamekuwa kero kubwa na kusababisha shughuli za uzalishaji mali kuzorota.
Amesema serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imesikia kilio cha wananchi na imeanza kuchukua hatua ili kuhakikisha usalama wa wananchi unakuwepo muda wote na kwamba, jukumu la kuwavuna wanyama hao litasimamiwa na maofisa na askari wa wanyamapori.
Comments